Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, November 13, 2012

LIONEL MESSI AVUNJA REKODI YA MABAO YA PELE

LIONEL MESSI AVUNJA REKODI YA MABAO YA PELE


BARCELONA, Hispania
Mabao 76 aliyofunga, ni tisa nyuma ya Gerd Muller anayeshikilia rekodi ya kudumu, wakati Pele alikuwa akishika nafasi ya pili – akiwa ametikisa nyavu mara 75 akiwa na klabu yake ya Santos na timu ya taifa ya Brazil mwaka 1958
MWANASOKA Bora wa Dunia kwa miaka mitatu mfululizo, Lionel Messi, juzi amethibitisha kuwa ni bora kuliko nyota wa zamani wa soka duniani Edson Arantes do Nescimento ‘Pele’ na hilo ni rasmi kwa sasa na halina mjadala.
Messi nyota wa klabu ya FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentine, ameivunja rasmi rekodi ya mabao ya Pele shujaa wa Brazil – aliyofunga kwa upande wa klabu na timu ya taifa katika kalenda ya mwaka.
Mkali huyo aliye katika kinyang’anyiro cha kuwania tuzo ya nne mfululizo ya Balon d’Or, alifunga mara mbili katika ushindi wa Barca wa mabao 4-2 dhidi ya Mallorca na kumfanya afikishe idadi ya mabao 76 kwa mwaka huu wa 2012.
Idadi hiyo, ni mabao tisa nyuma ya Gerd Muller anayeshikilia rekodi ya kudumu, wakati Pele alikuwa akishika nafasi ya pili – akiwa ametikisa nyavu mara 75 akiwa na klabu yake ya Santos na timu ya taifa ya Brazil mwaka 1958.
Kocha wa Barca, Tito Vilanova hakusita kuizungumzia rekodi hiyo, akisema: “Rekodi ya Leo ni ya kuvutia mno.
“Ni ya kuvutia zaidi wakati unapofikiria juu ya ukweli kwamba, amefunga mabao mengi zaidi kwa mwaka, ambao kimsingi haujaisha.
"Baadhi ya wachezaji ufunga idadi hiyo ya mabao katika kipindi cha misimu kati ya saba hadi nane, yeye amethubutu kufanya hivyo katika mwaka mmoja. Na mengi kati ya hayo ni mabao ya ufundi zaidi.”
Messi mwenye rekodi ya kusisimua dimbani katika misimu saba mfululizo ya ligi, anaongoza mbio za Kiatu cha Dhahabu msimu huu akiwa na mabao yake 15, huku akiwa ametikisa nyavu mara 20 katika mashindano yote ya msimu huu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...