Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 9, 2014

MBUNGE MGIMWA AZINDUA VICOBA IHEMI

Mbunge  wa  jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akizindua kikundi  cha VICOBA cha Igunga na Amkeni Group kata ya Ihemi
Mbunge  wa  jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akikabidhi mchango  wake wa Tsh 700,000 kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za vicoba jimboni
……………………………………………………………………….. 
Na Francis Godwin Blog.

WANACHAMA  wa  vikundi  vya Vicoba  Igunga na Amkeni Group kata ya Mgama katika Halmashauri ya  Iringa   wamempongeza mbunge  wa  jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa  kwa  kuviwezesha  vikundi  hivyo mtaji  kwa ajili ya kuwawezesha  wanachama  hao kukopeshana  zaidi.

Mratibu  wa  Vicoba mkoa wa  Iringa Thisiana Kikoti alitoa  pongezi hizo leo  wakati uzinduzi  wa Vicoba katika kijiji  cha Ihemi  .
Kikoti  alisema  kuwa uanzishwaji wa vikundi  hivyo ni  jitihada za aliyekuwa mbunge wa  jimbo la Iringa mjini Monica Mbega ambae  alihamasisha  kuanzishwa kwa  VICOBA mkoani Iringa na katika  jimbo la Kalenga hamasa ya kuanzishwa kwa  vikundi  hivyo  imefanywa na aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo marehemu Dr Wiliam Mgimwa na sasa jitihada  zinazofanywa na mbunge  wa  sasa Godfrey Mgimwa ni  wazi zitafanikisha kukua kiuchumi kwa  wananchi  wa  jimbo hilo.

Alisema  kuwa  lengo  ni kuona  inaanzishwa bendi  ya  VICOBA kwa  ajili ya  kuwawezesha  wananchi zaidi  kiuchumi. Huku  kwa  upande  wake  mbunge Mgimwa  mbali ya  kuchingia  kiasi  cha Tsh 700,000 pia  alisema  kuwa  ndoto ya  mbunge aliyefariki wa  jimbo hilo ilikuwa ni kuanzisha  benki ya maendeleo katika  jimbo la kalenga  na kuwa tayari  alianza  kuandika andiko na suala hilo ataliendeleza .
wakati  huo  huo  mbunge  huyo  ameahidi  kuchangia  kiasi  cha shilingi 700,000 kwa  vikundi vya Ihekima ,tugele na Imani vyenye  wanachama 80 kwa  ajili  ya  kuviwezesha  zaidi
vikundi  hivyo vina akiba  ya shilingi milioni 8 toka vilipoanmzishwa  mapema  mwaka  huu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...