Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 16, 2014

UN KUZINDUA MFUMO MPYA WA KUHABARISHA UMMA NDANI YA TAMASHA LA ZIFF 2014 JIONI HII



un1
Ofisa habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vusso (kushoto) akionesha taarifa ya Umoja wa Mataifa ya utekelezaji wa mpango wa pamoja wa mashirika ya Umoja wa mataifa hapa nchini. Taarifa hiyo imo katika documentary (taarifa ambayo iko katika mfumo wa video) ya dakika saba inayoonyesha kazi mbalimbali Umoja wa Mataifa nchi itazinduliwa leo kwenye ukumbi wa Ngome Kongwe kuanzia saa moja jioni katika mpango wa Umoja wa Mataifa wa kutumia mitandao ya kijamii kuwafikia wadau wake wa maendeleo
Un2
Mkuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini Anna Liboro Senga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo kuhusu uzinduzi wa mfumo mpya wa utoaji wa taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa wadau wake.Mpango huo unazinduliwa leo jioni katika ukumbi wa wazi wa Ngome Kongwe. Kushoto ni Ofisa habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vusso .(Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...