Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 16, 2014

RAMBIRAMBI MSIBA WA GEORGE MPONDELA


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga, George Mpondela kilichotokea jana (Juni 15 mwaka huu) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa klabu ya Yanga, Marehemu Mpondela anatarajiwa kuzikwa Alhamisi (Juni 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, na msiba upo Kigamboni Mnarani.
Mpondela alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga katika uchaguzi uliofanyika mwaka 1994 baada ya kumshinda aliyekuwa mpinzani wake wa karibu George Ndaombwa.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu nchini kwani, Mpondela enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa akiwa kiongozi katika klabu yake ya Yanga.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Mpondela, na klabu ya Yanga na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Taratibu zaidi za mazishi zitatolewa na Yanga baada ya kufanya mawasiliano na familia ya marehemu Mpondela. Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...