Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, December 29, 2012

UBUNGO BUS TERMINAL KUHAMA JANUARY 15, 2013.


MCHAKATO wa kuhamisha Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi (UBT), kwenda Mbezi Luis unatarajiwa kuanza Januari 15 mwaka ujao.
 
Akizungumzana wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Jiji Mussa Zungiza, alisema lengo la kuhamisha kituo hicho ni kwa ajili ya kupisha Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART).
 
Alisema kuhamishwa kwa kituo hicho kutakuwa kwa awamu, kutakakokwenda sambamba na kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha Mbezi.
 
“Siyo kweli kama ifikapo Januari tunahamisha au tunasimamisha shughuli zote pale Ubungo la hasha, tutakacho fanya pale tutawakabidhi wajenzi wa mradi huo wa DART ambao nao watachagua maeneo maalumu ya kuanzia shughuli zao, huku maeneo mengine yakiendelea kutoa huduma bila ya kuleta athari katika utoaji huduma”alisema Zungiza.
 
Zungiza alisema hadi sasa pale Mbezi kinachofanyika usafishaji wa eneo hilo la stendi hiyo mpya. Alisema katika awamu hiyo ya kwanza watejenga miundombinu ikiwemo uzio, alama za kuelekeza magari, njia za kuingia na kutoka.
 
“Pengine tunatarajia ndani ya miezi mitano tunaamini awamu yakwanza itakuwa imekamilika”alisema.
 
Zungiza alisema uhamishaji kabisa wa kituo hicho cha Ubungo kutategemea kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho kipya cha Mbezi. 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...