Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, August 3, 2014

Chiku Gallawa mgeni rasmi Handeni Kwetu Foundation


MKUU wa Mkoa wa  Tanga, Chiku Gallawa anatarajiwa kuwa mgeni
rasmi katika uzinduzi wa taasisi ya Handeni Kwetu Foundation, utakaofanyika Jumanne ya Agosti 5, katika Ukumbi wa Vijana Social Hall,  Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo la uzinduzi wa taasisi hiyo limepangwa kuanza saa 10 za jioni ambapo wamealikwa wageni mbalimbali kwa ajili ya kuitambulisha kabla ya kuanza kazi zake rasmi nchini Tanzania.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa taasisi hiyo, Kambi Mbwana, alisema kuwa wameona wamualike RC Gallawa kuwa mgeni rasmi
kwakuwa ni miongoni mwa viongozi makini na wenye kiu ya maendeleo hapa nchini.

Alisema kuwa kitendo cha kuzinduliwa na Mkuu wa Mkoa Tanga, kinaonyesha namna gani viongozi wa serikali wanashirikiana na wadau wote kwa ajili ya kufanikisha mipango ya kimaendeleo.

“Tanzania imejaliwa kuwa na viongozi makini mno, hivyo taasisi imemualika Mheshimiwa Gallawa kuwa mgeni wake rasmi ili ashirikiane na wageni waalikwa kuitambulisha taasisi.

“Tunaamini kwa pamoja tutafanikisha kuitambulisha taasisi kwa
wadau wote, hususan Watanzania kwa kupitia Handeni Kwetu Foundation,
ukizingatia kuwa imesajiliwa kufanya kazi zake nchini nzima,” alisema.


Kwa mujibu wa Mbwana, sera na mikakati ya taasisi hiyo itaanikwa
katika utambulisho huo utakaokuwa na malengo mahususi ya kujikwamua kiuchumi na kuhamasisha masuala ya utawala bora.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...