Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, August 18, 2014

WASANII WA BONGO MOVIE WAWAOMBEA DUA WASANII WENZAO WALIOFARIKI DUNIA


Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi,Abdallah Bulembo (katikati) akiwasili katika viwanja vya karimjee jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuungana na wasanii kwenye dua maalum ya kuwaombea wasanii waliotangulia mbele ya haki.Kulia ni Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity,Steven Mengele maarufu kama Steve Nyerere.
Msanii wa vichekesho ambaye pia ni muinjilisti kwa sasa Emanuel Mgaya Maarufu kama Masanja Mkandamizaji akiongoza dua kwa upande wa wakristo huku Msanii Jacob Stephen JB akiwa ameishikilia Biblia.Kulia ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Alhaj Mussa Salum ambaye aliongoza dua kwa upande wa waislam,katika shuguli hiyo ya kuwaombea Wasanii waliotangulia mbele ya haki,iliyofanyika jana kwenye viwanja vya Karimjee,jijini Dar es salaam.
 Baadhi ya wadau wa Filamu nchini wakiwa kwenye shughuli hiyo ya kuwaombea Dua Wasanii wote waliotangulia mbele ya haki (waliofariki) iliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee,jijini Dar es salaam jana.
 Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Alhaj Mussa Salum akijadiliana jambo na baadhi ya wadau walioshiriki kwenye dua hiyo.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity,Steven Mengele maarufu kama Steve Nyerere akipeana mkono na watu mbali mbali baada ya kumalizika kwa dua ya kuwaombea wasanii waliotangulia mbele ya haki,iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee,Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...