Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, August 12, 2014

RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA KISIMA CHA MAJI, LAMBO KATIKA KIJIJI CHA JAMII YA WAFUGAJI CHA MBALA,CHALINZE


 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete akionozana na akina mama wa jamii ya kimasai waliobeba maji waliyoyateka baada ya mbunge huyo kuzindua kisima cha maji katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, Bagamoyo mkoani Pwani jana. Kisima hicho pamoja na lambo la kunyweshea mifugo vimejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. Kushoto ni Kiongozi wa mradi huo, Joseph Chagama na nyuma yake ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Ridhiwani Kikwete akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kisima hicho. Kushoto ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana.
 Ridhiwani akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa jamii ya kimasai baada ya kuzindua kisima hicho.
 Mama mwingine wa Jamii ya Kimasai akitwisha ndoo ya maji na Ridhiwani Kikwete

 Ridhiwani Kikwete akifungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua lambo la kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mbala kinachokaliwa kwa asilimia kubwa na jamii ya wafugaji
 Ng'ombe wakitoka kunywa maji kwenye lambo hilo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...