Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, September 14, 2013

TENGA AWATAKA WAHITIMU GRASSROOTS KUSAMBAZA UJUZI!!


Tenga-wa-TFFNa Boniface Wambura, TFF
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewataka wahitimu wa kozi ya ukocha wa grassroots kusambaza ujuzi walioupata nje ya shule zao ili mradi huo uwe na manufaa nchi nzima.
Akifunga kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 30 kutoka Tanzania Bara na Visiwani kwenye ukumbi wa TFF leo (Septemba 13 mwaka huu), Rais Tenga amewakumbusha kuwa mradi huo umelengwa kuenea nchi nzima katika kipindi cha miaka mitatu.
Mradi wa grassroots unalenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12, na kozi hiyo ilikuwa chini ya Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Govinder Thandoo kutoka Mauritius.
Washiriki waliohitimu kozi hiyo na kukabidhiwa vyeti ni Abdulkheir Khamis Mohamed (Kaskazini A), Ali Hamad Mohamed (Wete), Ali Khamis Ali (Wete), Amin Amran Yunus (Micheweni), Amina Mhando (Kibaha), Benito Mwakipesile (Kibaha), Deogratius Yesaya (Kibaha), Editha Katabago (Bagamoyo), Habiba Mulungula (Bagamoyo) na Irene Semng’indo (Kibaha).
Juma Omar Abdallah (Kaskazini A), Kassim Ibrahim Mussa (Mkoani), Khamis Haji Ali (Kusini Unguja), Khamis Hamad Rajab (Chakechake), Mahfoudh Abdulla Said (Wete), Marianus Nyalale (Bagamoyo), Maryam Suleiman Ali (Mjini Magharibi), Maryasa Juma Ali (Mjini Magharibi), Mohamed Ali Abdullah (Mjini Magharibi) na Mohamed Salim Omar (Micheweni).
Mohamed Seif Abeid (Mkoani), Ramadhan Kejeli (Bagamoyo), Rhobi Kibacho (Kibaha), Salim Suleiman Juma (Chakechake), Shaaban Naim Suleiman (Kusini Unguja), Shabani Rashid Masimbi (Bagamoyo), Talib Ali Rajab (Chakechake), Thabit Juma Makungu (Kusini Unguja), Yusuf Ali Issa (Mjini Magharibi), Zakia Choum Makame (Mjini Magharibi).
Hiyo ni kozi ya pili ya grassroots kufanyika nchini ambapo ya kwanza ilifanyika Desemba mwaka juzi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...