Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, September 27, 2013

MAONYESHO YA UWEKEZAJI KANDA YA KASKAZINI YALIYODHAMINIWA NA NMB YAFANA


photo1
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa Benki ya NMB Bi. Josephine Kulwa (kushoto) alipotembelea banda la NMB katika maonesho ya Uwekezaji Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika Jijini Tanga 26-27/9/2013. Walioambatana naye ni Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji Mhe. Dr. Mary Nagu, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kapteni Mstaafu Mh. Chiku Galawa, Mwenyekiti wa Mkutano wa Uwekezaji Nd. Salum Shamte pamoja na viongozi na washiriki wengine. photo2Naibu Waziri TAMISEMI Mh. Aggrey Mwanri akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembelea banda la NMB katika maonesho hayo. Kutoka kulia ni Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB Bi. Vicky Bishubo, Meneja Mawasiliano wa Benki ya NMB Bi. Josephine Kulwa pamoja na wafanyakazi wa NMB Tawi la Madaraka Tanga. photo3 
Mkurugenzi Ukaguzi wa ndani wa Makampuni ya Impala Bw. Julius Makara (kushoto) akipewa maelezo ya kuhusu Huduma Mbalimbali za Benki ya NMB toka kwa Meneja Mahusiano Mwandamizi wa Wateja Wakubwa Bw. Nsolo Mlozi baada ya kutembelea banda la NMB photo4Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Mulongo (kulia)akibadilishana mawazo na Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB Bi. Vicky Bishubo baada ya kutembelea banda la NMB. Kushoto ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Pangani Farms Bw. Charles Makoi.
photo5 Mkurugenzi Mtendaji wa Pride (T) Limited Bw. James Obama (kushoto) akipewa maelezo ya kuhusu Huduma Mbalimbali za Benki ya NMB toka kwa Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB Bi. Vicky Bishubo. Pembeni yake ni Meneja wa Tawi la NMB Madaraka Tanga Bw. Juma Mpimbi, Meneja Uwekezaji wa NSSF Bw. Abdallah Mseli na Meneja Mahusiano Wateja Wakubwa Bi. Shilla Senkoro katika maonesho hayo. photo6Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mh. Majid Mwanga (kati) akibadilishana mawazo na Meneja Mawasiliano wa Benki ya NMB Bi. Josephine Kulwa, Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB Bi. Vicky Bishubo baada ya kutembelea banda la NMB katika maonesho ya Uwekezaji Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika Jijini Tanga. Photo7Mbunge wa Kilindi Mh. Beatrice Shelukindo akiwa na maofisa wa NMB alipotembelea banda la NMB katika maonesho ya Uwekezaji Kanda ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...