Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 17, 2013

BFT: TUNASUBIRI BARUA KUTOKA AIBA KWAAJILI YA MASHINDANO YA KLABU BINGWA YA KIMATAIFA



Na Elizabeth John


SHIRIKISHO la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), linasubiri barua kutoka Shirikisho la Ngumi Duniani (AIBA) kwaajili ya kujulishwa tarehe mpya ya mashindano ya ubingwa wa Afrika ambayo yanatarajiwa kufanyika huko Mauritius.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Septemba mosi hadi 7 nchini humo kabla AIBA hawajahairisha kutokana na sababu ambazo zimeelezwa kwamba zipo nje ya uwezo wao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga alisema timu ya taifa inaendelea na mazoezi ya kujifua kwaajili ya mashinndano hayo katika uwanja wa ndani wa taifa.
“Timu ipo vizuri kwaajili ya mashindano hayo, bado inaendelea na mazoezi kama kawaida bado hatujajua ni lini mashindano hayo yataanza tunasubiri barua kutoka AIBA tukipata taarifa tutatangaza,” alisema.

Mashaga aliwaomba watanzania wajitokeze zaidi kusaidia timu yetu ya taifa ili uwakilishi katika mashindano ya kimatifa uwe wenye tija kwa kuzingatia kuwa watanzania wote ndio wanachohitaji na ili kitimie mabondia lazima waandaliwe vema.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...