Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, September 26, 2013

Azam Tv yamkosha Julio


KOCHA Msaidizi wa timu ya Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' ameipongeza kampuni ya Azam TV  kwa kitendo chao cha kuongeza udhamini katika Ligi Kuu Tanzania Bara, kitu alichodai kimesaidia kuongeza ushindani katika ligi tofauti na zamani.
Julio alisema udhamini huo wa Azam TV ambao umezihusisha timu zote umesaidia kuondoa ligi ya timu chache na ndiyo maana mpaka sasa kumekuwa na matokeo ya kushangaza hata kwa timu ambazo zilikuwa zikionekana kama nyonge.
Akizungumza na MICHARAZO, Julio alisema udhamini mpya wa Azam umezifanya kila timu kuwa na maandalizi mazuri na ari ya kutaka kufanya vyema katika ligi kitu ambacho kimesababisha baadhii ya timu zilizozoea 'kupeta' kuwa na wakati mgumu.
"Kama mdau wa soka naipongeza kampuni ya Azam Media kwa uamuzi wake wa kuongeza udhamini katika ligi, imeifanya ligi kuwa tamu na yenye ushindani wa kweli kitu ambacho kitasaidia kupanda kwa soka la Tanzania," alisema.
"Ule utamaduni wa timu ndogo kuwa wanyonge mbele ya timu kubwa ni kama sasa unaondoka na hiki ni kitu kizuri kwa mustakabali wa soka letu, hivyo nawapongeza na kutaka wengine wajitokeze kusaidia kuinua soka la Tanzania," aliongeza Julio.
Alisema anaamini ushindani uliopo katika ligi msimu huu utasaidia kutoa mabingwa na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kimataifa wanaostahili na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika anga hizo badalaya kuwa wasindikizaji tu,
"Ligi inapokuwa ngumu na yenye ushindani inasaidia kutoa mabingwa wa kweli na wanaostahili ambao wataiwakilisha vyema kimataifa, hivyo narejea kuipongeza Azam Media walichokifanya na kuomba wasapotiwe na kila mtu," alisema Julio.
Kampuni hiyo ya Azam Media imeingia mkataba wa kuidhamini Ligi Kuu Tanzania Bara wenye thamani ya Sh. Bilioni 6 ambapo kila klabu ya ligi itakuwa ikivuna Sh Milioni 100, hiyo ni mbali na udhamini wa wadhamini wakuu wa ligi hiyo Vodacom

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...