Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 30, 2013

Msiba Tena! Mac 2 B afariki, Watuguru naye katangulia


TASNIA ya sanaa nchini imeendelea kupata pigo baada ya mcharaza gitaa Joseph Watuguru na Mac Maliki Simba 'Mac 2 B wamefariki dunia siku ya leo.


Watuguru alifariki  katika hospitali ya Amana wakati Mac 2 B aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, mtayarishaji wa muziki huo na Reggae kufariki leo asubuhi nyumbani kwao Yombo kwa Abiola.

Mac 2B aliyekuwa membaz wa kundi la Wateule alikuwa akisumbuliwa na miguu mpaka mauti yalipompata nyumbani kwao Yombo na anatarajiwa kuzikwa kesho asubuhi.

Naye Watuguru aliyewahi kutamba na bendi mbalimbali ikiwemo African Revolution 'Tamtam' na Mchinga Sound alifariki kutokana na kuugua muda mrefu na inaelezwa kuwa huenda naye akazikwa kesho.

MICHARAZO inatoa pole kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na wadau wa sanaa kwa ujumla kwa misiba hiyo ambayo imekuja wakati tasnia hiyo ikiendelea kuomboleza vifo vya wasanii wengine waliotangulia mbele ya haki tangu mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...