Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, September 26, 2013

MPAMBANO MWINGINE WA MASUMBWI KUWAKUTANISHA CHEKA VS SHAURI OKTOBER 27


Mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka  wakitunishiana misuri wakarti wa utambulisho wa mpambano wao wa ubingwa wa UBO Dar es  salaam
utakaofanyika tarehe 27 mwezi wa kumi 
Promota wa Mpambano wa Ubingwa wa UBO Kaike Siraju katikati akiwanyoosha mikono juu mabondia Ramadhani Shauri kushoto na Cosmasi Cheka watakaopigana tarehe 27 Mwezi wa kumi  jijini Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
 

MPAMBANO WA mwingine wa masumbwi unatarajia kufanyika Oktoba 27 katika ukumbi wa Friends Coner  Manzese Dar es salaam litakalo wakutanisha mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka mpambano huo ulidhaminiwa na Hotel ya Tanamera ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani
 
Akizungumza mratibu wa mpambano huo Kaike Siraju amesema amepata sapoto katika hotel hiyo ili aweze kuendereza vipaji vya vijana unakumbuka mimi ndie ninae andaaga mapambano makubwa nchini kama utakumbuka ila nilisimama kidogo kwa ajili ya kutafakali na kulekebisha mambo yangu binafsi lakini kwa sasa nimekuja kuinua mchezo huu kwa vijana chipkizi kwanza ndio msingi wa ngumi duniani kote
 
aliongeza kwa kutaja mapambano ya utangulizi kuwa ni Mohamed Matumla anamenyana na Sadiki Momba huku Amosi Mwamakula akizichapa na Hamisi Ajali na Juma Fundi atazipiga na Shabani Kilumbelumbe
 
Siku hiyo kutakuwa pia na huzwaji wa DVD kali za ngumi wakiwemo mabondia wakali wanaotamba Duniani na hapa nchini kama.Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Floyd Mayweathar,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
 
DVD hizo za ngumi kali zitakuwa zikiuzwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'
 
Pamoja na kutambua sheria na taratibu za mchezo huo siku hiyo pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo huo wa masumbwi vitakavyotolewa  zawadi kwa mabondia na Kocha Super D  ambaye ame haidi kutoa, Gum Shit ,Clip Bandeji,DVD za Mafunzo kwa mabondia, Bukta,Protector na vifaa mbalimbali kwa mabondia watakao onesha uwezo wa ali ya juu wa kutupiana masumbwi

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...