Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 23, 2013

Kipigo chaiporomosha Yanga, mabao 76 yafungwa mpaka sasa


Mabingwa watetezi
WAKATI mabingwa watetezi Yanga wakijikuta wakiporomoka kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara hadi nafasi ya nane toka ile ya nne iliyokuwapo awali kabla ya pambano lao la leo dhidi ya Azam, jumla ya mabao 76 yameshatinga wavuni hadi sasa ligi ikiwa katika raundi ya tano.
Yanga imesaliwa na pointi zake sita na ikiwa nyuma ya wageni wa ligi hiyo Mbeya City yenye pointi saba, huku Azam na Coastal zikizipumulia maafande wa Ruvu ambazo zote zilichezea vichapo katika mechi zao leo.
Vinara Simba wanaendelea kusalia kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 11 na mabao yao 13 ya kufunga na kufungwa magoli manne, huku JKT Ruvu ikifuatia ikiwa na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa ikiizidi Azam licha ya kulingana nao pointi 9 sawa na Ruvu Shooting na Coastal Union.
Azam yenyewe imefunga mabao nane na kuruhusu mabao matano, wakati JKT Ruvu imefunga mabao sita na kufungwa mawili na kuwa, ikifuatiwa na ndugu zao Ruvu Shooting waliofunga mabao sita na kufungwa matatu kisha Coastal iliyofunga magoli matano na kuruhusu nyavu zake zitikiswe mara mbili.
Kagera Sugar iliyoanza ligi kwa kusuasua ushindi wake wa jana dhidi ya Ashanti umeiweka katika nafasi ya sita ikiwa na pointi nane na kufuatiwa na Mbeya City wenye pointi saba kisha Yanga yenye pointi zake sita.
Oljoro JKT iliyokuwa nafasi ya pili toka mkiani imechupa hadi nafasi ya 11 mwa msimamo baada ya ushindi wake wa leo dhidi ya JKT Ruvu ikifikisha pointi nne na kuirithisha nafasi hiyo Prisons-Mbeya huku Ashanti wakiendelea kuzibeba timu zote 13 za ligi hiyo ikiwa na poingti moja tu.
Mpaka sasa ligi ikijiandaa kuingia raundi ya sita siku ya Jumatano kwa pambano moja tu kati ya Rhino Rangers ya tabora itakayoialika Ashanti United mjini Tabora jumla ya mabao 76 yameshatinga wavuni, huku Tambwe Amissi wa Simnba akiongoza orodha ya wafungaji wenzake akiwa na mabao sita.
Tambwe anafuatiwa kwa mbali na washambuliaji nyota wa Yanga, Jerry Tegete na Didier Kavumbagu na Haruna Chanongo, mchezaji wenzake wa Simba wenye mabao matatu kila mmoja.
Angalia msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa na orodha ya wafungaji pamoja na ratiba ya mechi zijazo.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014      
                                    P  W  D  L   F   A  GD  PTS
1.  Simba                      5   3   2   0  13  4    9   11
2.  JKT Ruvu                5   3   0   2   6   2    4    9
3.  Azam                       5   2   3   0   8   5    3    9
4.  Ruvu Shooting          5   3   0   2   6   3    3    9
5.  Coastal Union          5   2   3   0   5   2    3    9
6.  Kagera Sugar           5   2   2   1   6   3    3   8
7.  Mbeya City              5   1   4   0   5   4   1    7
8.  Yanga                       5   1   3   1  10  7   3   6
9.  Mtibwa Sugar           5   1   3   1   3  4   -1   6
10.Rhino Rangers           5   0   4   1   5  7   -2   4
11.Oljoro                       5   1   1   3   3   6  -3   4
12.Mgambo                   5   1   1   3   2  10 -8   4
13.Prisons                      5   0   3   2   2   8  -6   3
14.Ashanti                      5   0   1   4   2  11 -6   1

Wafungaji:

6- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete , Didier kavumbagu (Yanga), Haruna Chanongo (Simba),
2- Jonas Mkude (Simba), Jerry Santo (Coastal Union),Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Paul Nonga (Mbeya City), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, Haruna Moshi (Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Hamis Kiiza (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, Kipre Tchetche, John Bocco, Joseph Kimwaga (Azam), Mwagani Yeya, Steven Mazanda, Richard Peter (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally, Shaaban Nditi (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Themi Felix, Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Godfrey Wambura, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa (Oljoro JKT)

Mechi zijazo
Sept 25, 2013
Rhino Rangers vs Ashanti Utd

Sept 28, 2013

Yanga vs Ruvu Shooting
Rhino Rangers v Kagera Sugar
Mbeya City vs Coastal Union
Mgambo JKT vs Oljoro JKT

Sept 29, 2013

Ashanti Utd vs Mtibwa Sugar
JKT Ruvu vs Simba
Prisons vs Azam

Matokeo ya mechi zilizopita ni kama ifuatavyo:

Ratiba ya Ligi Kuu 2013-2014
DURU LA KWANZA
Agosti 24, 2013
Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013
Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)

Sept 18, 2013
Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Sept 21, 2013
Mgambo JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Prisons vs Mtibwa Sugar (1-1)
Simba vs Mbeya City (2-2)
Kagera Sugar vs Ashanti United (3-0)

Sept 22, 2013
JKT Ruvu vs Oljoro JKT (0-1)
Azam  vs Yanga (3-2)
Coastal Union v Ruvu Shooting (1-0)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...