Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 9, 2013

Zidane amkataa Bale Madrid



Kiungo mshambuliaji mpya wa Real Madrid, Gareth Bale ameanza kukutana na joto ya jiwe klabuni hapo baada ya Kocha msaizidi wa timu hiyo, Zinedine Zidane kutokubali usajili ghari wa mchezaji huyo.
Mkongwe huyo ambaye aliwahi kuichezea klabu hiyo alisema jana kuwa hakubaliani ya mchezaji huyo kutoka Tottenham Hotspur kusajiliwa kwa dau kubwa la pauni 85.3 milioni kwani kiwango chake hakiendani na fedha hizo.
Bale, 24, alijiunga na Madrid Septemba mosi na kuvunja rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa kwa fedha nyingi rekodi iliyokuwa ikishindikiwa na Cristiano Ronaldo aliyesajiliwa na klabu hiyo akitokea Manchester United mwaka 2009 kwa ada ya uhaimsho ya pauni 80 milioni.
"Miaka 10 iliyopita nilinunuliwa kwa pauni 48 milioni na nilisema kuwa sikustahili kununuliwa kwa fedha hizo," alisema Zidane. "Sasa nafikiria pia kuwa mchezaji hawezi kustahili kununuliwa kwa kiasi hicho cha pesa. Huu ni mpira wa miguu, sielewi nini kinatokea hadi mchezaji ananunuliwa kwa fedha nyingi kiasi hicho."

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...