Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, August 10, 2012

WAYNE ROONEY AMUITA ROBIN VAN PERSIE MANCHESTER UNITED


 Robin van Persie kushoto na Wayne Rooney kulia
 Robin van Persie akishikilia tuzo yake ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya England
 Robin van Pesrie kushoto akisalimiana na Wayne Rooney katika moja ya mechi kati ya Arsenal na Man United
LONDON, England

MSHAMBULIAJI mahiri wa kimataifa wa England, Wayne Rooney, ametoa mwito kwa Mholanzi Robin van Persie kuungana naye klabuni Old Trafford yaliko makazi ya Manchester United.
Bosi wa Mashetani Wekundu hao, Mskochi Sir Alex Ferguson, anahaha kupata saini ya Van Persie nahodha na mshambuliaji tegemeo wa Arsenal kwa dau la pauni mil. 20, huku Gunners ikionekana dhahiri kumbania.
Washika Bunduki chini ya Mfaransa Arsene Wenger wameonesha kutokuwa tayari kumuuza RVP kwa mahasimu wao wa Ligi Kuu ya England, ingawa United mara kadhaa imetoa msisitizo wa kumuhitaji na kutaka kuwapo kwa mazungumzo.
Rooney anayetamani kuunda pacha na Van Persie katika safu ya mbele ya Man United, alisema: “Bila shaka, yeye ni mchezaji ninayevutiwa naye. Amekuwa na kiwango cha kustaajabisha nakuvutia akiwa Arsenal kwa miaka kadhaa sasa.
“Msimu uliopita unaweza kuwa ndio bora zaidi kwake, kwani alifunga mabao mengi. Kama atakuja hapa, anaweza kuwa na mchango mkubwa kwa kikosi na mafanikio makubwa.”
Alipoulizwa kama angependa kufanya kazi pamoja na RVP katika safu ya mbele United, Rooney alitabasamu na kujibu: “Ningependa kufikiria hivyo, lakini unapaswa kumuuliza kocha juu ya hilo.
“Kuna fowadi wengi hapa ambao wanacheza nami ama nafasi yangu, kuna Welbeck (Danny), Chicharito na Berbatov (Dimitar) bado yuko hapa pia. Hivyo kuna washambuliaji kibao wanaopigania nafasi hapa,” alimaliza Rooney.
Van Persie amekana kurefusha mkataba wake Emirates akidaiwa kukimbia njaa ya mataji kwa misimu saba sasa na Rooney anabainisha kuwa lengo kuu la klabu yake ni kurejesha taji lililotwaliwa na majirani zao Manchester City katika siku ya mwisho ya msimu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...