Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, August 12, 2013

Hatimaye yathibitika Sheikh Ponda kujeruhiwa kwa risasi angalia picha zake


Jeraha la Sheikh Ponda linavyoonekana kwa karibu

Sheikh Ponda akiwa hospitalini


Sheika Ponda akiwa wodini Muhimbili

BAADA ya danadana ya Polisi kukwepa ukweli juu ya tukio la kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda, ukweli sasa upo hadharani baada ya kiongozi huyo wa Umma wa Kiislam kuonesha jeraha hilo hadharani akiwa kalazwa Muhimbili.
Awali Polisi mkoa wa Morogoro kupitia Kamanda wake Faustin Shilogile lilikuwa likidai halijui lolote kuhusu tukio hilo, licha ya kukiri kwamba ilitaka kumkamata kiongozi huyo kipenzi wa waislam walio wengi.
Tangu jana vyombo vya habari vikitumia vyanzo vyake vya habari kutoka mjini humo ikiwemo MICHARAZO viliripoti juu ya tukio hilo ambalo lilitokea jioni mara baada ya Sheikh huyo kuhutubia kwenye Kongamano la Kiislam, lakini Polisi ikawa inavunga kuwa haujui lolote.
Hatimaye sheikh huyo alitua jijini mchana kwa matibabu katika hospitali ya Muhimbili na 'kuwaumbua' wale waliokuwa wakikanusha taarifa hizo kwamba hakuna kilichotokea juu ya kujeruhiwa kwake.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amezungumza jijini Dar leo na kumtaka Rais Jakaya Kikwete na IGP Saida Mwema kuangalia namna ya kuthibiti jeshi la Polisi juu ya matumizi ya risasi za moto kwa raia wasio na silaha yoyote.
Matukio ya polisi kuwatwanga risasi raia kwa sasa imekuwa kama fasheni, kitu ambacho kinawatia hofu raia juu ya umakini wa askari wa jeshi hilo ambalo ni la usalama wa raia na mali zao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...