Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, August 1, 2013

NEY WA MITEGO ATUMA 'SALAMU ZAO’



Na Elizabeth John

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Emmanuel Elibariki ‘Ney wa Mitego’ Anatarajia kuachia kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Salamu zao’ hivi karibuni.

 Ney wa Mitego ni kati ya msanii ambaye anafanya vizuri katika soko hilo, na pia anasema ameamua kufanya kazi hiyo kwa lengo la kuburudisha na kuwaelimisha wapenzi wa kazi zake.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Ney wa Mitego alisema kazi hiyo anatarajia kuanza kuisambaza wiki ijayo ambapo kwa sasa anatarajia kuanza ‘kushuti’ picha mbalimbali kwa ajili ya video ya kazi hiyo.

“Wiki hii naanza kushuti katika sehemu mbalimbali, mashabiki wanatakiwa kuupokea vizuri wimbo huu kwani ni bonge la kazi, kama wanavyonijua mashabiki wangu sijawahi kufanya vibaya katika kazi zangu, naomba tu wakae mkao wa kula kwaajili ya kazi hiyo,” alisema Ney wa Mitego.


Msanii huyo ambaye kwasasa anatamba na kibao chake cha ‘Nasema nao’, aliwaomba mashabiki waipokee kazi hiyo kwani ina ujumbe mzito kwa jamii yote

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...