Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, February 10, 2011

TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA LINALOZAMINIWA NA KAMPUNI YA ZANTEL LAZINDULIWA RASMI

MISS UALII 2011 WAEMBELEA UDIZUNGWA

Hapa wakiwa katika hifadhi ya tarangire
Washiriki wa utalii wakicheza kutafuta miss utalii tarangire
Baadhi ya washiriki wa miss utalii wakiwa wamepunzika katika hifadhi ya Tarangire
Hapa wakiwa katika maporomoko ya mlima udizungwa

Wednesday, February 9, 2011

MASHINDANO YA NYAMA CHOMA YAZINDURIWA

Meneja wa Bia ya Safari Lager,Fimbo Buttallah (kati) akifafanua jambi wa wakti wa uzinduzi wa mashindano ya kuchoma nyama yajulikanayo kama "Safari Lager Nyama Choma"katika pub iliyopo ndani ya kampuni ya bia Tanzania,jijini Dar.kulia na kushoto ni majaji wa mashindano hayo.

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imezindua rasmi yale mashindano ya aina yake na ya kuvutia ya kuchoma nyama yajulikanayo kama “Safari Lager Nyama Choma”

Mashindano haya hushirikisha majiko ya baa mbalimbali katika umahiri wa kuchoma nyama na hatimaye zawadi hutolewa kwa washindi.

Akizungumza katika uzinduzi wa mashindano ya mwaka huu, meneja wa Bia ya Safari Lager Bw. Fimbo Butallah alisema; madhumuni makubwa kwa bia ya Safari lager kuendesha mashindano haya ambayo yamekuwa kivutio kwa walaji wa nyama na watumiaji wa bia ni kuhakikisha tunaleta changamoto kwa majiko yanayochoma nyama, ili kuhakikisha walaji wanapata kile kilicho bora kabisa. Watumiaji wa bia ya Safari Lager, hupendelea sana kuitumia huku wakisindikiza na nyama choma iliyoandaliwa vizuri, hivyo kupitia mashindano haya, bia ya Safari Lager inaendeleza utamaduni wa kunywa bia na kula nyama. Kufuatia ubora wa hali ya juu wa bia ya Safari lager, tunafurahi sana pale ambapo mywaji atapata pia nyama iliyo bora ili mtumiaji aweze kuridhika zaidi.

Mashindano ya mwaka huu yatafanyika katika mikoa mine ambayo ni; Dar Es Salaam, Kilimanjaro, Arusha na Mbeya. Kuna ongezeko la mkoa wa Mbeya ambao mwaka juzi haukushiriki. Ni matarajio ya bia ya Safari Lager kuyapeleka mashindano haya katika mikoa yote siku za usoni.

Akitaja zawadi za washindi, Butallah alisema; baa itakayoshika nafasi ya kwanza itajinyakulia shilingi Milioni Moja, mshindi wa pili, Laki Nane, Mshindi wa Tatu laki Sita, Nafasi ya Nne; Laki Nne na nafasi ya Tano shilingi Laki Mbili. Zawadi hizi zimegawanywa kwa kila mkoa.

Utaratibu wa kupata baa zitakazoshiriki mashindano haya utaendeshwa kwa njia ya simu, ambapo wananchi watatakiwa kutuma ujumbe mfupi usemao “Safari kisha Mkoa uliopo ikifuatiwa na jina la Baa” kisha tuma kwenda namba 15540. Utapokea ujumbe kukuhakikishia kuwa kura yako imepokelewa. Jopo la majaji litapitia kura zote na Baa Tano zitakazokuwa zimepata alama za juu zaidi ndizo zitakazopambana katika eneo la wazi ambapo mandhari ya kula nyama na kunywa bia itakuwa imeandaliwa.

Vigezo vitakavyoangaliwa na majaji katika mashindano haya ni pamoja na Usafi wa eneo, vifaa na muhusika, uchaguzi wa nyama, maandalizi ya nyama, jinsi ya uchomaji, muda unaotumika, jinsi nyama inavyofikishwa kwa mlaji na Ladha. Baa zitakazofanikiwa kuingia katika kinyang’anyiro zitapewa semina elekezi juu ya vigezo hivi kabla ya mpambano.

TOT PLAS KUIBUKIA VALENTINE DAY

Kundi zima la Tot Plus Taarab, siku ya Wapendanao 'Valentine Day', yaani tarehe 14/2/2011, litarindima katika ukumbi wa Traverine Hotel, Magomeni jijini Dar es Salaam, katika onyesho maalum la kuzindua albamu yake mpya ya 'TOP IN TOWN', kwa maelezo zaidi tafadhali soma bango lao hilo kwa makini.

WASANII WA TAARAB WAKIWA KAZOEZINI LEO


KIONGOZI wa kundi la TOT Plus Taarab, (wapili kulia) akiongoza baadhi ya wasanii wa kundi hilo kufanya mazoezi, leo katika ukumbi wa CCM, Mwinjuma, Dar es Salaam, jana. Mazoezi hayo ni kwa ajili ya uzinduzi wa albamu mpya ya kundi hilo ya 'Top in town' utakaofanyika Jumatatu, ijayo, katika ukumbi wa hoteli ya Travertine, Magomeni. Wengine kushoto ni Aziza Jumaa, Rukia Juma na Hemedi Omari.
Mwanamtama Amir na Sharifa Mohammed wakiwa kwenye mazoezi hayo
Kutoka kushoto, Mwasiti Suleiman, Omari Ali 'Kopa Jr', Mariam Khamis ak paka mapepe wakiwa katika mazoezi hayo
Rukia Juma, akifanya mazoezi
Tahabiti Abdul akicharaza kinanda kwenye mazoezi hayo
http://bashir-nkoromo.blogspot.com/

Tuesday, February 8, 2011

RAY KUTOKA NA FILAMU YA NYUMBA NDOGO


MSANII wa filam nchini Vicent Kigisi Ray nyota wa fani hiyo nchini yupo mbioni kuachia kutoa kazi nyingine itwayo 'The Sacond Wife' filamu hiyo ya kimapenzi imewashilikisha wasanii nyota kadhaa pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibukia katika fani hiyo filamu hiyo iliyotaalishwa na Kampuni ya RJ.Prodution Ni Miongoni wa waigizaji walioshiliki ni Ray,mwenyewe,Colleta Raymond,Aisha BUI,Riyana Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwaye Aisha ambaye ni chipukizi Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa filamu hiyo ambayo amigiza kama muumini wa kislam ipo hatua ya mwisho kabla kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii. 'Kama nilivyofanya kwenye offside kwenye Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yaleyale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata huondo' alisema Ray kwa mujibu wa taalifa hizo kama filamu zake nyingine, The Seco Wife' itasambazwa na Kampuni ya Steps Entertainment.

Sunday, February 6, 2011

SIKINDE WATESA NA BONANZA LA KONYAGI


Waimbaji wa bendi ya Sikinde wakitoa burudani wakati wa bonanza linalozaminiwa na Konyagi linalofanyika kila jumamosi katika ukumbi wa DDC Kariakoo

TIMU YA TAIFA YA PALESTENA YATUA KUIKABILI TAIFA STARS

Balozi wa Palestina Nchini Dr. Nasri Abu Jaish mwenye suti nyeusi katikati akiwa na wachezaji wa timu ya taifa hilo baada ya kuwasili Dar es salasam leo







Wachezaji wa timu ya taifa ya Palestina wakiwasili katika Uwanja wa ndege wa KImataifa wa Julius Nyerere, Dar es salaam leo kwa ajili ya mpambano wao dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania


NILIPOKUWA TUNAWASUBILI WAPALESTINA KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU NYERERE LEO

Friday, February 4, 2011

VIDEO YA SUPER D BOXING COACH KUTOKA HIVI KARIBUNI


BONDIA wa Zamani na Kocha wa Ngumi wa Klabu ya ngumi ya Ashanti, Rajabu Mhamila
'Super D' yupo mbioni kutoa Video inayozungumzia maisha yake ya mchezo huo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Super D alisema video hiyo itakuwa sokoni muda
wowote kuanzia sasa ikizungumzia maisha yake tangu alipoanza kucheza mchezo huo
mwaka 1984 hadi 2010 sasa.
Alisema Video hiyo itaonesha mapambano mbalimbali aliyocheza na dhidi ya
mabondia Mbwana Matumla, Rashidi Ali na Ajibu Salumu.
Alisema lengo la kuandaa video ni kutaka kutimiza malengo yake ya kuendeleza
mchezo wa ngumi kwa kuwapatia vijana nafasi ya kujifunza kupitia kwake.
Alisema kutokana na nchi ya Tanzania kuwana vipaji vingi atashindwa kuwafikia
kila mmoja wao na badala yake amewapa fursa ya kujifunza kwa kuangalia video.
Alisema Video katika kuhaikisha Video hiyo inafanya vizuri sokoni ameongezea
vionjo vingine kutoka kwa mabondia maarufu duniani kama Mike Tyson, Michael Mo,
Junior Myweather, Mohamed Ally, Man Paqyao na Joe Fleizer.

WATU MIA MOJA KUPIMWA MACHO NA KUFANYIWA UPASUAJI BULE


JUMUIYA ya Mabohora nchini itafanya upasuaji wa macho bure ikiwa ni maadhimisho ya kusherehekea miaka 100 ya kuzaliwa shekhe wao Dkt. Syedna Mohammed Burhanuddin.

Mjumbe wa Kamati ya maadhimisho hayo, Bw. Saifuddin Jamal alisema jana kuwa watu wote wenye matatizo ya macho wanatakiwa kujiorodhesha katika hospitali za Amana, Temeke, Mwananyamala na Amtulabai ya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Bw. Jamal alisema wagonjwa watakaofanyiwa upasuaji ni 100 kutoka sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam watakaowahi kujiandikisha katika hospitali hizo zilizotajwa baada ya kuidhishwa na madaktari wa hospitali hizo.

"Waliogundulika kuwa wana matatizo ya macho ya mtoto wa jicho na presha ya macho watafanyiwa upasuaji Februari 7 hadi 10 kwenye hospitali ya Burhani na daktari Dkt. Mustafa Parekt kutoka India anayetarajia kuwasili kesho kutwa (Jumapili)". alisema.

Alisema wenye matatizo hayo yanaweza pia kujiandikisha katika hospitali ya Burhani ambako upasuaji huo utafanyika kwa wastani wa wagonjwa 25 kwa siku.

ALLY CHOKI AIBOMOA TWANGA PEPETA

KIongozi wa kundi la Extra Bongo Ally Choki akiwa na wasanii nane aliowapata kutoka Twanga Pepeta na kuwatambulisha mbele ya wana habari leo

WAMACHINGA WA KICHINA KUANZA KUKAMATWA KESHO

Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Cyril Chami
Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Cyril Chami (kushoto) akitoa tamko la kukamatwa kwa wafanyabiashara wa kigeni wanaofanya kinyume na sheria katika eneo la Kariakoo Dar es salaam jana kazi hiyo ya kuwakamata inanza leo kulia na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Bw. Lazaro Nyalandu

BOT YATETEA NOTI ZA 'BATIKI'


BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa ufafanuzi kuhusu utowaji wa rangi katika noti mpya na kusema kuwa hali hiyo ni ya kawaida kwa noti zilizochapwa kwa teknolojia maaluum ijukanayo kama 'Intaglio Printing'

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alisema aina hiyo ya uchapishaji unafanya noti kuwa na hali ya mparuzo zinapopapaswa na imetumika ili kuimarisha kingo za noti kwa lengo la kupunguza uwezekano wa kuchanika na kuchakaa kwa haraka.

Prof.Ndulu alisema miparuzo hiyo huacha rangi noti inaposuguliwa kwa nguvu kwenye karatasi nyeupe kitendo ambacho kinathibitisha kuwa noti hiyo ni halali.

"Kutoa rangi ni moja ya arama ya usalama inayothibitisha kuwa noti siyo bandia,noti hizi hazichuji zikilowekwa kwenye maji kama inavyodaiwa kwa kuwa wino uliotumika hauyayuki katika maji"alisema Prof.Ndulu

Prof.Ndulu alisema kuwa utowaji wa rangi huo upo hata katika noti za nje kama dola pale zinaposuguliwa ambapo teknolojia iliyotumika kutengezewewa inalingana.

Alisema kuwa noti hizo zimetengenezwa kwa teknolojia ya kuwekewa kinga dhidi ya uchafu ili kupunguza uwezekano kunasa uchafu inapokuwa katika mzunguko.

Aliongeza kuwa noti za zamani bado ni halali na zitaendelea kutumika pamoja na zile mpya mpaka zitakapopotea katika mzunguko kwa sababu ya uchakavu wake.

Akizungumzia kuwepo kwa noti mmoja iliyo na thamani kubwa zaidi ya sh.10,000/- alisema BoT haikuona haja ya kufanya hivyo kwakuwa malipo makubwa yanahimizwa kufanywa kupitia njia ya nyingine za kibenki kama njia ya mitandao.

Thursday, February 3, 2011

WABUNGE WA MKOA WA RUVUMA WAKUTANA KUPANGA MPANGO MKAKATI DAR LEO

Wabunge wa Mkoa wa Ruvuma wakiwa kwenye kikao cha mpango mkakati Dar es salaam leo kutoka kushoto ni Eng. Stella Manyanya,Eng.Ramo Makani, Dkt. Emanuel Nchimbi na Jenista Mhagama

Wednesday, February 2, 2011

ZANTEL YAZINDUA MNARA WA HUDUMA ZA INTANET BUKOBA

Mkuu wa mkoa wa Kagera Mohamed Babu akikata utepe kuzinduwa mnara mpya wa Zantel wa huduma za intaneti jijini Bukoba. Pembeni kwake ni Mkuu wa kitengo cha mahusiano ya umma na matukio wa Zantel William Mpinga.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mohamed Babu akitumia huduma ya intaneti ya Zantel baada ya hafla fupi ya kuuwasha mnara mpya wa intaneti eneo la Kibeta, Bukoba. Pembeni yake ni Mkuu wa kitengo cha mahusiano na matukio wa Zantel William Mpinga.

SHIRIKA LA NYUMBA LATOA SIKU 26 KWA WADAIWA SUGU KULIPA MADENI YAO

Mkurugenzi wa Matawi na Utawala wa Shirika la Nyumba la Taifa Bw. Raymond Mndolwa akitangaza uamuzi wa shirika hilo kutoa muda wa hadi tarehe 28 mwezi huu kwa wadaiwa wa shirika hilo kulipa madeni yao, kinyume na hapo shirika hilo litachukua hatua ya kutoa vitu vyao vya ndani na kuvipiga mnada. Kushoto ni Mkuu wa Elimu kwa Umma na Huduma kwa Jamii Bi. Susan Omari.

NMB YATOA MSAADA WA MABATI SHULE YA MSINGI SINZA

Meneja Mwandamizi Huduma kwa Biashara ya Serikali(NMB) Bi. Domina Feruzi (katikati) akikabidhi msaada wa mabati kwa Afisa Elimu kata ya Sinza Bi. Phoibe Ileta kwa niaba ya shule za Msingi za Sinza na Sinza Mashujaa. Kushoto ni Mwenyekiti wa Shule ya Msingi Sinza Bw. Flavian Mgori.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Sinza wakitoa burudani ya ngoma.

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB.

Wanafunzi wa Shule za Msingi za Sinza na Sinza Mashujaa zilizopokea msaada wa mabati hayo.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...