Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, March 26, 2013

ABOMOLEWA NYUMBA NA KUCHOMEWA VYOMBO VYA NDANI AKIDHANIWA MSHIRIKINA ILEMI MBEYA


Wananchi wenye hasira kali wakibomoa nyumba ya mama Atupele Kalile akidhaniwa kuwa mchawi maeneo ya ilemi Mbeya
Kazi ya kubomoa nyumba ya mama huyo inaendelea
Wengine wameshaingia ndani na kuanza kutoa vyombo nje tayari kwa kuvichoma
Mtoto wa mama Atupele akijaribu kuokoa vitu vya mama yake visichomwe moto na wanakijiji
Vyombo vinazidi kutolewa ndani ilivichomwe moto
Tayari wameshaanza kuchoma moto vyombo vya mama Atupele
Mwingine anaendelea kubomoa nyumba ya mama Atupele
Wamefyeka shamba lake lote la mahindi
Wengine wanapongezana kwa kazi waliofanya
Kushoto mama Atupele Kalile anaedhaniwa kuwa ni mshirikina akiwa na mtoto wake





MWANAMKE mmoja aliyejulikana kwa jina la Atupele Kalile (60) mkazi wa Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi Jijini Mbeya amenusurika kifo baada ya wananchi wa Mtaa huo kutaka kumpiga kisha kubomoa nyumba yake wakimtuhumu kwa ushirikina.
  
Wananchi hao kumtuhumu Mwanamke huyo kuhusika na upotevu wa motto mwenye umriwa miaka mitatu(3) (Judith Chengula) aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha Februai 22, Mwaka huu.
  
Kwa mujibu wa wakazi hao walisema Mtoto huyo alipotea majira ya saa 11 jioni baada ya kupoteana na dada yake  Anitha Mgaya wakiwa wametokea kanisani ambapo hadi sasa mototo huyo hakuweza kupatikana licha ya juhudi kubwa za wakazi hao kumtafuta bila Jitihada.
  
Walisema katika vikao kadhaa vilivyoitishwa mtaani hapo kwa ajili ya kutafuta mbinu za kupatikana kwa mtotolakini Mwanamke huyo hakuonesha ushirikiano jambo ambalo lilizua hofu miongoni mwa wakazi hao hali iliyopelekea kuhisiwa kuhusika na tukio hilo.
  
Walisema katika kikao kilichofanyika Machi 23 Mwaka huu majira ya Asubuhi mtaani hapo wananchi hao waliendelea kusisitiza kuwa Mwanamke huyo achukuliwe hatua kwa kuwa ndiye anayehusika na upotevu wa motto ambapo iliamriwa kwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi.
  
Walisema baada ya kufika nyumbani kwake na kufanya upekuzi walikuta vitu vinavyohisiwa kuwa vinahusika na ushirikina ambavyo ni vitovu vya watoto wachanga watatu ambapo Mwanamke huyo baada ya kuulizwa alishindwa kutolea ufafanuzi hali iliyosababisha wananchi kupandwa na hasira na kuanza kumpiga.
  
Kutokana na tukio hilo Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo Nedy Mwamlima alimnusuru Mwanamke huyo katika kipigo kutoka kwa wananchi kwa kumpeleka katika kituo kikuu cha Polisi kwa usalama zaidi.
  
Baada ya mtuhumiwa huyo kunusuriwa na kukimbizwa katika kituo cha Polisi wananchi hao hawakupoza jazba zao ambapo waliamua kuteketeza nyumba ya mtuhumiwa ikiwa ni pamoja na kufyeka mazao yaliyokuwa yamepandwa jirani na nyumba yake.
Hata hivyo hasira za wananchi hao hazikuishia hapo bali walimsakama Mwanamke mwingine aliyejulikana kwa jina la Agnes Sika ambaye ni mke wa Mchungaji wa kanisa la Pentecost Groly  kwa madai kuwa ni rafiki wa mtuhumiwa na amekuwa akimfichia siri.
  
Jeshi la Polisi liliwahi kufika eneo laTukio na kumnusuru Agnes asipatwe na madhara ikiwa ni pamoja na kutochomewa nyumba yake ambayo tayari wananchi hao walionekana kuikimbilia kwa ajili ya kutaka kuibomoa.
  
Aidha Jeshi la polisi linaendelea kumshikilia mtuhumiwa kwa ajili ya mahojiano zaidi pamoja na upelezi ambapo Baba mzazi wa Mtoto anayesadikiwa kupotea katika Mazingira ya kutatanisha akisema anamwachia Mungu  baada ya juhudi za kumtafuta kushindikana.


picha na E. Kamanga

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...