Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, December 28, 2013

FUMANIZI KRISMAS HILI HAPA


KRISMASI noma sana! Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Baba Pendo ameiona chungu Sikukuu ya Krismasi 2013 kufuatia tukio la kufumaniwa na mkewe, Mama Pendo au Mama P ‘akibanjuka’ na mwanamke ndani ya gari.

NI MKESHA WA KRISMASI
Tukio hilo la aina yake lilijiri eneo maarufu Kijitonyama jijini Dar linalojulikana kwa jina la Miti Mirefu, usiku wa Mkesha wa Krismasi, majira ya saa 8:00 usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.
Ina maana kwamba Baba Pendo aliamua ‘kumalizia shida’ zake ndani ya gari hilo ambalo namba zake za usajili tunaziweka kapuni.


OFM YAJUZWA
Kabla ya tukio hilo, mara kadhaa Mama P aliwasiliana na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers na kulalamika juu ya mumewe kutoka nje ya ndoa na mwanamke mmoja wa mjini.
Mama P: Haloo…naongea na OFM? Jamani naombeni mnisaidie kuna mwanamke anamzuzua sana mke wangu.
OFM: Una uhakika mama?

Mama P: Nina uhakika wa asilimia mia moja. Hapa nimeona meseji wamepanga kukutana leo na ndiyo maana nikawatafuta. Ninyi mpo wapi?
OFM: Sawa, sisi tupo kikazi Mango Garden (Kinondoni, Dar) wewe upo wapi?
Mama P: Nipo Sinza A (Dar) nitawashtua mambo yakiiva maana najua lazima mume wangu atatoka muda si mrefu, nimemuona anajiandaa.

OFM: Oke lakini uwe makini sana.
Mama P: Sawa, nitawashtua.
Hiyo ilikuwa saa 5:12 usiku, hivyo OFM iliendelea na majukumu mengine ya kufichua uovu katika jamii.

BABA PENDO AAGA ANAKWENDA MKESHA
Kwa mujibu wa Mama P, majira ya saa 5:20 usiku, mumewe alimuaga anakwenda kwenye mkesha wa kumpokea mwana wa Mungu (Yesu) aliyezaliwa ambapo kwa mujibu wa mume huyo, alikuwa anakwenda kusali Kanisa la Mtakatifu Maximilian Kolbe lililopo Mwenge, Dar.

MAMA P MZIGONI
Baada ya mumewe kuondoka, mwanamke huyo aliwasiliana na OFM na kuwapa ishu nzima ambapo walimpa mbinu ya kumfuatilia mumewe ikiwa ni pamoja na kubadili aina ya usafiri ili asishtuke.

Mama P alichukua Bajaj na kumfuatilia mumewe hadi maeneo ya Sinza-Kijiweni ambapo alimuona akipaki gari lake na kuingia kwenye ‘pabu’ moja kisha akaagiza ‘ngumu kumeza’ (mzinga wa konya) ambayo aliipiga taratibu hadi mishale ya saa 8: 05 usiku huku akipiga stori na washkaji.
Baada ya hapo, Baba Pendo aliingia garini kuondoka. Mama P naye akachukua bodaboda kumfuatilia kwa nyuma.
Alipofika maeneo ya Kijitonyama  alimuona akisimamisha gari na kuingia kwenye ‘kamtaa’ f’lani, akatoka na mwanamke kisha akaingia naye kwenye gari.
Alisema yeye akiwa bado nyuma, walipofika Miti Mirefu  mumewe alipaki gari lakini hakuna aliyeshuka.

Aliendelea kusimulia kisa mkasa mbele ya ‘kachero’ wa OFM kuwa uvumilivu ulimshinda, alihisi kuna linaloendelea ndani ya gari,  akaamua kulisogelea na ndipo hamadi! Akamkuta mumewe ‘laivu akiduu’ na mwanamke huyo na ndipo OFM walipochomoza baada ya kujulishwa kuwa ishu imetiki.
“Uzuri ni kwamba walisahau ‘kuloki’ milango ya gari ‘so’ nilipoushika ukafunguka,” alisema Mama P baada ya OFM kupiga picha za kutosha.

TIMBWILI
Katika tukio hilo kulitokea timbwili ambapo askari waliokuwa doria walitonywa na kufika eneo la tukio na kuamulia damu isimwagike.
Mwanamke aliyenaswa na mume wa mtu alikula mbata za kufa mtu huku mwanaume akitoka nduki kukwepa aibu ya kamera za OFM.

MAMA P HASIRA
OFM ilimsikia Mama P akisema: “Kumbe ndiyo wewe…nilikuwa nakufuatilia muda mrefu, badala ya kwenda kanisani unahangaika na waume za watu hata humuogopi Mungu.”

Hadi gazeti hili linaondoka eneo la tukio, wanawake hao walikuwa mikononi mwa polisi wakitakiwa kuacha ugomvi na kama kuna malalamiko wayafikishe

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...