Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, December 28, 2013

STENDI YA NJOMBE JIMBONI KWA SPIKA MAKINDA YALALAMIKIWA

Abiria   wakipita kwa shida katika  stendi ya  Njombe 
Mwanahabari  wa Clouds TV na Radio Recho akitafuta  eneo la  kupita  katika  stendi  hiyo ya Njombe 
Madereva  na  abiria   wanaotumia  stendi ya Njombe mjini  ambayo ni stendi kuu ya mabasi  yaendayo mikoani  wamelalamikia  ubovu  wa stendi  hiyo na kumwomba  mbunge wa  jimbo  hilo Anne  Simamba  Makinda  kushughulikia  tatizo  hilo.

Wakizungumza na mtandao  huu wa www.francisgodwin.blogspot.com  madereva hao na  wananchi  walisema  kuwa  ubovu wa stendi  hiyo umekuwa ni kero kubwa  kwao  na  kuiomba  Halmashauri  ya  mji  wa Njombe  kulishughulikia  suala   hilo

John Sanga  ni  mmoja  kati ya madereva  eneo hilo la stendi alisema kuwa  wameshangazwa na hatua ya  mbunge  wao ambae ni spika wa Bunge  kushindwa  kuwajibika kwa kusimamia utengenezaji wa  stendi hiyo.

Kwa  alisema  wakati wa jua  eneo hilo limekuwa  likiongoza kwa  kuwa na  vumbi na  wakati wa masika  linaongoza kwa kuwa na tope sana .

Hata   hivyo  alisema  kuwa uongozi  wa serikali ya  Njombe  umekuwa ukitoa ahadi ya  kutengeneza stendi  bila kutekeleza kwa wakati na pale  madereva  wanapotaka  kugoma wamekuwa  wakitumia polisi  kuwakamata  waanzilishi  wa migomo  hiyo.

Huku Sarah Ndelwa ambae  ni mmoja kati ya abiria   waliohojiwa akimtaka  mbunge Makinda  kusaidia  kuondoa aibu hiyo ya ubovu wa  stendi  nyumbani kwake

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...