Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, December 25, 2013

REDDS MISS TANZANIA 2013 KUSHEREHEKEA SIKUKUU YA X MASS NA WATOTO YATIMA KITUO CHA MGOLOLE MOROGORO


Redds Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa (pichani), tarehe 25 Desemba 2013 atajumuika na watoto yatima wa kituo cha Mgolole Orphanage kilichopo Bigwa nje kidogo ya Mji wa Morogoro.
 
Mrembo huo ataungana na warembo wengine watatu, akiwemo Miss Tanzania mshindi wa pili Latifa Mohamed, Miss Tanzania mshindi wa tano Elizabeth Perrty, na Sabra Islam Miss Morogoro 2013 ambaye ndie atakae kuwa mwenyeji wao wakati wote wakiwa mkoani hapo.
 
Ni kawaida kwa Mrembo wa Taifa, Miss Tanzania kila mwishoni mwa mwaka kula X Mass na Watoto Yatima, wasiojiweza pamoja na wale waishio katika mazingira magumu.
 
Baada ya shughuli hiyo Miss Tanzania Happiness Watimanywa atajumuika pia na watoto wa aina hiyo jijini D’salaam siku ya Mwaka mpya tarehe 1 January 2014 katika vituo vingine atakavyopangiwa na  Kamati ya Miss Tanzania.
 
Pamoja na shughuli hiyo, Mrembo Happiness Watimanywa pia anakusudia  kusaidia jamii wenye matatizo ya Maji kwa kuwachimbia visima vya maji safi katika mikoa ya Dodoma na Singida.
 
Miss Tanzania Happiness Watimanywa ambaye pia ni Miss Dodoma na Miss Kanda ya Kati 2013, ambaye pia ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu  nchini Scotland ameahirisha masomo yake kwa muda wa mwaka mmoja hadi hapo atakapovua Taji la Mrembo wa Taifa mwishoni mwa mwaka ujao 2014.
 
 
 
HIDAN .O. RICCO.
PUBLIC RELATIONS OFFICER
LINO INTERNATIONAL AGENCY
 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...