Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, April 18, 2014

MAMA SALMA APOKEA MBIO ZA PIKIPIKI KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUNGANO-ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA LINDI


 Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mtwara ndugu Mohamed Sinani  akikabidhi picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa Mama Salma Kikwete na picha ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mheshimiwa Abeid Aman Karume kuashiria muendelezo wa mbio za uzalendo za pikipiki kusherehekea miaka 50 ya Mungano wa Tanganyika na Zanzibar hapo.
 Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mtwara Ndugu Mohamed Said Sinani (mwenye kofia) akifuatana na viongozi wenzake wa Chama Cha Mapinduzi na Umoja wa Vijana kwenda kukabidhi mbio za pikipiki kwa uongozi wa Mkoa wa Lindi kwenye Kijiji cha Madangwa jana.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)  wa Lindi Mjini na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimsikiliza kwa makini mtoto Idd Omar kutoka katika Kijiji cha Madangwa , kata ya Sudi huko Lindi Vijijini. Mama Salma alifika kijijini hapo kwa ajili ya kupokea mbio za uzalendo za pikipiki zilizoandaliwa na Umoja wa Vijana, (UVCCM) kitaifa zikitokea Mkoa wa Mtwara.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...