Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, April 20, 2014

MTOTO ALIYEIBWA AKABIDHIWA KWA WAZAZI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi akimkabidhi kwa mama yake mzazi mtoto Goodluck mara baada ya kupatikana

Akipokea Mtoto wake Mama mzazi Mboka Mwakikagile(20) amelishukuru Jeshi la polisi na wananchi wema kwa kufanikisha kupatikana kwa mtoto wake  Goodluck Salehe aliyeibwa na Askari wa Jeshi la Polisi WP 5367 Prisca Kilwai April 6, mwaka huu huko Kasumulu wilayani Kyela.


 Mtoto  Goodluck Salehe 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi,akizungumza baada ya kukabidhi mtoto huyo aliwasihi wazazi kuwa makini na utunzaji wa watoto ili kuepuka vitendo kama hivyo kujirudia.





Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi akizungumza na shangazi wa mtoto aliyeibiwa pembeni ni baadhi ya waandishi wa habari walioshuhudia makabidhiano hayo




BAADA ya Jeshi la Polisi mkoani Mbeya  kumtia nguvuni Askari wake anayetuhumiwa kuiba mtoto wilayani Kyela,Mtoto huyo akabidhiwa kwa wazazi wake huku wakiendelea na uchunguzi zaidi.
Makabidhiano hayo yamefanyika   katika Hospitali ya Wazazi Meta alikokuwa akipatiwa matibabu mtoto huyo katika chumba cha Joto na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi.
Akipokea Mtoto wake Mama mzazi Mboka Mwakikagile(20) amelishukuru Jeshi la polisi na wananchi wema kwa kufanikisha kupatikana kwa mtoto wake  Goodluck Salehe aliyeibwa na Askari wa Jeshi la Polisi WP 5367 Prisca Kilwai April 6, mwaka huu huko Kasumulu wilayani Kyela.
Aidha mwanamke huyo amemshukuru zaidi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi pamoja na Askari wengine  waliofanikisha mtoto wake kupatikana akiwa hai.
Baadhi ya ndugu waliofurika katika Hospitali ya Meta kushuhudia makabidhiano hayo wamesema hawaamini  kile kilichotokea baada ya kuwa katika hofu takribani siku kumi na moja baada ya kuibwa katika zahanati ya Njisi iliyopo Kasumulu Kyela.
Aidha ndugu hao wamelipongeza Jeshi la Polisi kwa kufanikisha kupatikana mtoto na wasamaria wote walioshirikiana nao katika maombi hata kufanikisha upatikanaji wa mtoto huyo akiwa salama salimini.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi,akizungumza baada ya kukabidhi mtoto huyo aliwasihi wazazi kuwa makini na utunzaji wa watoto ili kuepuka vitendo kama hivyo kujirudia.
Ameongeza kuwa Jeshi la polisi bado linafanya upelelezi na kukusanya ushahidi zaidi ili waweze kuwafikisha mahakamani watumiwa kujibu mashtaka wanayokabiliana nayo.
Amesema Mtoto huyo alipatikana Aprili 17, mwaka huu akiwa na Askari huyo majira ya saa nne asubuhi  na kuongeza kuwa mpaka sasa sababu za kuiba mtoto huyo hazijafahamika na atafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya kuhukumiwa kijeshi.
Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...