Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, April 8, 2014

TBL YAFANIKISHA UPANDAJI MITI 1250 CHUO KIKUU CHA MOUNT MERU ARUSHA



 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Maunt Meru, mkoani Arusha Mchungaji Profesa Harrison Olang' (kulia), akishikana mikono na Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL), Bw. Devis Deogratius, baada ya kampuni hiyo kutoa miti 1300 kwa ajili ya mkoa wa Arusha, ambapo miti 1250 ilipandwa Chuoni hapo na miti 50 ilipandwa kwenye kiwanda cha TBL.

 Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), mkoani Arusha Bw. Devis Deogratius (aliyepiga magoti), akishiriki kupanda moja ya miti 1250 iliyotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya mkoa wa Arusha, baada ya kampuni hiyo kutoa miti 1300 kwa Manispaa ya Arusha, ambapo miti 1250 ilipandwa Chuoni hapo na miti 50 ilipabswa kwenye kiwanda cha TBL Arusha.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Maunt Meru, mkoani Arusha Mchungaji Profesa Harrison Olang' (aliyepiga magoti kushoto), akishiki kupanda miti 1250 chuoni hapo, iliyotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kwa ajili ya Manispaa ya Arusha. Wanaoshuhudia katika picha ni baadhi ya wafakazi wa TBL na wafanyakazi wa Chuo hicho.
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Bi. Stella Kaaya akishiriki kupanda moja ya miti 1300 iliyopandwa katika Chuo Kikuu cha Maunt Meru, mkoani Arusha, iliyotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). 
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Bi. Stella Kaaya (kulia) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Maunt Meru mkoani Arusha Mchungaji Profesa Harrison Olang' (kushoto), baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti 1300 kwenye eneo la Chuo hicho, iliyotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...