Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, February 16, 2014

Semsekwa, Sharapova wafunika Extra Bongo

RAPA mpya wa Extra Bongo Grayson Semsekwa na mnenguaji Asha Shara juzi walifanikiwa kukonga nyoyo za mamia ya mashabiki wa muziki wa dansi waliojitokeza katika onyesho maalum la utambulisho wa wanamuziki hao lililofanyika katika Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar es Salaam. Semsekwa na Sharapova walitangazwa mwishoni mwa wiki iliyopita kujiunga na Extra Bongo wakitokea bendi hasimu ya African Stars Twanga Pepeta tayari kujiandaa na uzinduzi wa albamu mpya ya bendi hiyo inaoitwa Mjini Mipango itakayozinduliwa Februari 22 mwaka huu katika Ukumbi wa Dar Live Mbagala. Mara baada ya Mkurugenzi wa bendi hiyo Ally Choki kumpandisha jukwaani repa huyo na kuanza kuimba vipande vya rapu zake za kwenye nyimbo za zamani kama Regina Zanzibar, Double Double, 3x3 wadau mbalimbali walijikuta wakishindwa kutulia vitini na kuanza kumtunza hali iliyofanya Ukumbi mzima kuchangamka kwa mayowe ya furaha. Kwa upande wake Sharapova alionyesha umahiri mkubwa wa kunengua sambamba na wenzake katika shoo maalumu ya kinadada ambapo licha kutofanya nao mazoezi aliweza kuendana na staili za mtindo mpya wa bendi hiyo 'Kimbembe'. wanamuziki hao wanaonguna na wenzao tayari kuingia kambini wiki hii kujiwinda na uzinduzi wa albamu ya 'Mtenda Akitendewa' unaosuburiwa kwa hamu na mashabiki wa muziki wa dansi. Mtenda Akitendewa ni albamu ya nne kwa bendi hiyo iliyoasisiwa kwa mara kwanza mwaka 2003 ikiwa na waimbaji Ally Choki, Bashiri Uhadi, Bob Kissa, Richard Maarifa, Khalidi Chokoraa, Flora Moses, rapa Greyson Semsekwa, (solo) Bonzo Kwembe, Efraim Joshua,George Gama (besi) Rythm na kinanda Thabit Abdul drum (ngoma) zikipigwa na Imma Chokolate. Albamu ya kwanza iliitwa '3x3' ambao ni wimbo uliokuwa kwenye albamu nyimbo nyingine ni 'Regina Zanzibar', 'Tuchunge Wazazi au Fikiri Madinda', 'Nunu Milenium' 'Walimwengu Remix' na 'Odise'. Albamu ya pili ilitwa 'Bullet Proof' ikiwa na nyimbo kama 'Double Double' na 'Regina Zanzibar' kabla ya kusambaratika mwaka 2004 na bendi hiyo kuanzishwa tena mwaka 2009 na kuibuka na 'Mjini Mipango'. 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...