Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, February 24, 2014

MWAKA WA KILIMO WA AFRIKA WAZINDULIWA KANING'OMBE JIMBO LA KALENGA IRINGA


Mkurugenzi wa ANSAF, Audax Rukonge alipokuwa akieleza maudhui ya siku ya Mwaka wa Kilimo wa Afrika

Ukaguzi wa shamba la mfano katika kijiji cha Kaning'ombe ulifanywa
Wasanii, Mrisho Mpoto na Profesa J ambao ni mabalozi wa kampeni ya "Kilimo Kinalipa, Jikite" walikuwepo

Naye Mwakilishi wa shirika la Afrika One kutoka Afrika Kusini alikuwepo kuelezea kilimo kinavyoweza kuwatoa watanzania

Msanii Dokii naye alisema mambo na jinsi kilimo kinavyomtoa

Wazee wa kampeni, Mrisho Mpoto, Profesa J na Masoud Kipanya walisema maneno yao kwa kupokezana wakieleza jinsi kilimo kinavyoweza kuwa mkombozi kama dhamira itakuwepo

 
Mkulima wa mfano, Eusebio Mbagile alizungumzia changamoto wanazopata wakulima wadogo katika shughuli hiyo ya kilimo

Baada ya kueleza changamoto zinazowakabili, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine Ishengoma aliishia kwa kupata ka KUKU ka zawadi ili akale yeye na familia yake

JUKWAA la Wadau wa Kilimo (ANSAF) limekumbushia ahadi  ya kutenga asilimia 10 ya bajeti ya nchi kwa ajili ya Kilimo, iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete mwaka 2012.

Mkurugenzi wa ANSAF, Audax Rukonge aliyasema hayo leo wakati Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal aliyewakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dk Christine Ishengoma akizindua Mwaka wa Kilimo wa Afrika.

Uzinduzi wa mwaka huo unaokwenda na kampeni iliyopewa jina la ‘Kilimo Kinalipa, Jikite’ ilifanyika katika kijiji cha Kaning;ombe, wilayani Iringa mkoani Iringa.

Mbali na ANSAF, wengine wanaoratibu kampeni hiyo ni mashirika ya Cloud Media na Afrika ONE inayowataka viongozi wa Afrika kutimiza Azimio la Maputo linalohimiza uwekezaji katika kilimo

Mabalozi wa kampeni hiyo, wasanii maarufu, Mrisho Mpoto, Profesa J na Masoud Kipanya walizungumzia namna kilimo kinavyoweza kuwakwamua vijana na lindi la umasikini huku msanii wa filamu nchini Dokii akieleza mafanikio yake ya kilimo katika shamba lake lililoko wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Mkurugenzi wa ANSAF, alisema kwa kupitia azimio hilo la Maputo wakuu wa nchi walikubalina watenge bajeti ya asilimia 10 ya bajeti zao kwa ajili ya kilimo.

Alisema kiwango hicho kilitarajiwa kutosha kuchangia kuongeza uzalishaji na tija, kukuza sekta ya kilimo kwa asilimia 6 kwa mwaka na kuondoa tatizo la njaa na umasikini.

“Leo hii ni miaka 10 tangu makubaliano ya Maputo. Ni nchi nane tu za Afrika zimetimiza ahadi hiyo; Tanzania haimo katika nchi hizo,” alisema bila kuzitaja.

Alisema tafiti zinathibitisha kuwa kilimo huchangia mara 11 zaidi katika kuondoa umasikini ikilinganishwa na uwekezaji mwingine.

Alisema kama taifa limedhamiria kuondoa umasikini ni lazima kukipatia kilimo mtazamo mpya wa kiuchumi, usiokuwa na chembe za kisiasa huku uwekezaji ukifanywa kwenye maeneo ya kimkakati.

Katika hotuba yake kwa wadau wa Kilimo, Makamu wa Rais alisema kilimo ni lazima kiendelezwe kwa usalama wa chakula na maisha.

Alisema program ya kuendeleza kilimo ilizinduliwa mwaka 2005/2006 ikilenga kilimo kikue kwa asilimia sita kutoka asilimia nne ya hivisasa.

Alisema kwa kushirikisha sekta binafsi program hiyo inalenga pia kuwatoa wakulima katika kilimo cha kujikimu ili kiwe cha kibiashara.

“Tunatakiwa kuwa na muda maalumu wa kushughulikia ahadi ya Maputo ya kutenga asilimia 10 ya bajeti ya serikali, kufanya mabiliko ya sera na kuongeza uwajibikaji katika sekta hiyo,” alisema.

Mmoja wa wakulima wa mfano katika kijiji hicho, Eusebio Mbangile alisema shughuli ya kilimo ni kero kubwa kwa wakulima wadogo kutokana na ukubwa wa bei za pembejeo, upatikanaji wake na masoko.

Alisema “ninazo heka 45; ninazolima ni 19, wakati wa masika 15 na wakati wa kiangazi heka nne, kwa wastani natumia karibu Sh Milioni 4 kwa shughuli nzima ya kilimo kila mwaka;” alisema huku akionesha mashamba yake hayo ya mahindi.

Alisema kwa wastani hupata gunia 25 za mahindi kwa kila heka ambayo hata hivyo huwa hauzi kwa vipimo vinavyokubalika kisheria.

Alisema walanguzi wamekuwa wakinunua gunia la mahindi lenye ujazo wa kilo 150 hadi 160 kwa Sh 38,000 tu hali inayowapa hasara kubwa na kuwafanya waendelee kuwa masikini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...