Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, February 27, 2014

Titina wa Extra Bongo ajiandaa kuacha kunengua


Mnenguaji Titi Mwinyi 'Titina' akiwa katika pozi
MNENGUAJI mahiri wa bendi ya Extra Bongo, Titi Mwinyiamir maarufu kama 'Titina' amesema anajipanga kuachana na fani hiyo baada ya kuitumikia kwa zaidi ya miaka 10.
Akizungumza na MICHARAZO, Titina aliyewahi kutamba na Double M Sound, Twanga Pepeta na FM Academia, alisema anataka kuachana na fani hiyo ili kujikita kwenye uimbaji.
Titina alisema muda aliotumika kama dansa tangu mwaka 2000 umeufanya mwili wake kuchoka na sasa anadhani ni muda muafaka kuhamia kwenye uimbaji ili kuendeleza kipaji alichonacho.
"Natarajia kuachana na unenguaji ili nijikite kwenye uimbaji, kipaji hicho ninacho tangu utotoni sema kunengua kuliniathiri na kukisahau, ila sasa sina jinsi zaidi ya kukiendeleza," alisema.
Dansa huyo alisema tayari ameanza mazoezi ya kuimba ili akiwiva vyema ahamie huko kufuata nyazo za akina Tshallah Mwana na Mbilia Bel waliowahi kutanga kwenye unenguaji kabla ya kuhamia kwenyue uimbaji na kuishika Afrika.
Titina, alisema anaamini bidii yake katika kujifunza kuimba kwa sasa ndiko kunakoweza kumfikisha pale walipofikia wakali hao kutoka Kongo au baadhi ya wanamuziki wa kike wanaotamba nchini kama akina Luiza Mbutu na wengine ambao walianzia kwenye unenguaji kabla ya kuwa waimbaji.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...