Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, February 6, 2014

KITUO CHA MATANGAZO CHA TELEVISHENI CHA AFRIKA KUENDELEA KUELIMISHA JAMII YA KIISLAMU


 Mkurugenzi wa Kituo cha Matangazo ya Televisheni cha Afrika (Africa TV) Bwana Muharami Iddiss akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Cheti maalum cha  Africa TV cha kuitumia ZBC – TV kurusha Vipindi vyake.
Makamu wa Pilio wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Africa TV ulioambatana na baadhi ya Viongozi wa Taasisi za Dini mara baada ya mazungumzo yao yalioyofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar. Kulia ya Balozi Seif ni Mkurugenzi wa Africa TV Bwana Muharami Idriss na Kushoto yake ni Mshauri wa Africa TV HAPA Zanzibar Bwana Kassim Haidar Jabir.
*********************************************
Uongozi wa Kituo cha Matangazo ya Televisheni cha Afrika { Africa TV } wenye Makao Makuu yake Nchini Sudan umenasihiwa  kuendelea kufanya kazi zake  za kuelimisha jamii hasa umma wa Kiislamu kwa kuheshimu  maadili ya kazi zao ili kufanikisha vyema majukumu yake katika utaratibu uliojipangia.

Nasaha hizo zimetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati akizungumza na Uongozi wa Afrika TV ulioambatana na baadhi ya Viongozi wa Taasisi za Dini ya Kiislamu ambao upo Zanzibar kujitambulisha rasmi ukijiandaa na utaratibu wa   kutangazwa matangazo yake kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar { ZBC - TV }

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...