Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, February 15, 2014

Sikinde yapiga mbizi baharini na kuibukia Kigamboni


Baadhi ya wapiga wa Sikinde wakiwajibika

BENDI kongwe ya muziki wa dansi, Mlimani Park 'Wana Sikinde' leo inatarajia kuvuka bahari ya Hindi na kwenda kufanya onyesho maalum la Siku ya Wapendanao 'Valentine Day' eneo la Mji Mwema Kigamboni.
Onyesho hilo litafanyika kufcuatia maombi ya wadau wa muziki wa dansi wa eneo hilo ambao wanataka kuishuhudia bendi hiyo ikifanya vitu vyake huko kwenye siku hiyo ambayo husherehekewa kote duniani Februari 14 ya kila mwaka.
Mratibu wa onyesho hilo, Michael Yona alisema kuwa amesikia maombi ya wakazi wa Kigamboni na sasa anawapelekea bendi hiyo kongwe ambayo ana uhakika itawaburudisha vya kutosha kwenye siku hiyo maarufu duniani.
"Sikinde wana nyimbo zao mpya kama Kiboyo, Nundu ya Ng'ombe, Kukatika kwa Dole Gumba, Jinamizi la Talaka, Tabasamu Tamu, Deni Nitalipa na nyingine nyingi ambazo nina uhakika itakuwa ni nafasi ya pekee kwa wakazi wa Kigamboni kuburudishwa na nyimbo hizo," alisema Yona.
Alisema kuwa nyimbo hizo ndizo zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu mpya baada ya ile ya 'Supu Imetiwa Nazi' ambayo hadi sasa bado iko sokoni wakati wanamuziki wakiendelea kukuna vichwa ili kukamilisha vitu vipya.
Naye katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo alisema Sikinde alisema kuwa kwa muda mrefu haijafanya onyesho Kigamboni na kwamba ana uhakika wakazi wa eneo hilo wana hamu ya kuwaona Sikinde wakiwaburudisha.
"Kwanza kabisa ieleke kwamba Mlimani Park ni bendi ya watu wote wakiwamo wakubwa na vijana wadogo ambao naamini watakuja kuishuhudia kwenye onyesho hili la Siku ya Wapendanao," alisema Milambo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...