Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, January 17, 2013

FILAMU YA REAL PROMISE KUTOKA HIVI KARIBUNI



Na Elizabeth John
KAMPUNI ya Faisal Production ikiwa miongoni mwa taasisi chache zenye lengo maalum la kuhakikisha fani ya filamu inastawi na kupata maendeleo nchini, imeandaa kazi mpya inayokwenda kwa jina la ‘Real Promise’.

Katika filamu hiyo ambayo tayari imeanza kuwa gumzo la jiji, waigizaji nyota kama Mohammed Mwikongi ‘Frank’, Rose Ndauka, Bambucha na Rania wameshiriki na kufanya makubwa ambayo yatamfanya mtazamaji kutopata muda wa kufanya shughuli nyingine.

Kwa mujibu wa msemaji wa kampuni hiyo, Mohammed Njiriku, filamu hiyo kwa sasa iko katika hatua ya uhariri, akisisitiza kutoa tungo bora kabisa sambamba na kuchezwa vizuri na wahusika.

Real Promise inazungumzia mikasa ya mapenzi na hatua mbalimbali za kukabiliana nayo ikizingatiwa kuwa mapenzi ni sehemu kubwa ya maisha ya kila siku ya binadamu.

Rose, ambaye ameng’ara katika filamu nyingi hapa nchini, amefanya makubwa katika kazi hiyo inayotarajiwa kutoka wakati wowote mwezi huu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...