Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, April 3, 2013

BARRACK YOUNG CONROLLERS YA LIBERIA AMBAO NI WAPINZANI WA AZAM WATUA WAKIWA NA MATUMAINI KIBAO


Wachezaji wa Barack Young Controllers wakiwa na Afisa wa Shirikisho la soka nchini, Mzee Mshangama baada ya kutua uwanja wa ndege leo asubuhi


Wakipanda basi lao


Kocha mkuu Robert Lartey



Kocha na wachezaji ndani ya basi tayari kwa safari ya hotelini



Mtoto wa Rais wa Liberia  Robert Alvin Sirleaf , aliyevaa koti la suti akiwa na mmoja wa mtu ambaye alikuwa kwenye msafara


Wakishuka kwenye basi kuingia hotelini

Wakiwa ndani ya Saphirre court hotel

TIMU ya Barrack Young Controllers II ya Liberia imetua leo asubuhi huku ikiwa na matumaini kibao ya kuwafunga wapinzani wao Azam FC.

 Naye kocha wa timu hiyo, Robert Lartey, amejigamba kuwa uwezo wa kuifunga Azam FC kwenye mchezo wa marudiano wa  kombe la Shirikisho utakaochezwa jijini Dar es Salaam jumamosi kwani makosa yaliyoigharimu timu amekwisha yafanyia marekebisho

 “Mchezo huu ni muhimu kwa timu yangu na naamini nitashinda”, alisema Lartey.

Pia alijigamba kuwa na kikosi chenye wachezaji wenye vipaji ambao pia wapo timu ya taifa ya Liberia ya Vijana, akina Ezekiel Doe, Benjamin Gbamy na George Dauda.
Wachezaji wa timu hiyo wameonekana kuwa nyuso zao kutokuwa na furaha sijui ni kwa kutafakari kuwa walipoteza mchezo wa awali wakiwa nyumbani na sasa wanacheza ugenini.

Young Controllers imetua leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2:30 kabla ya muda wa 3.35 asubuhi ambao ulitarajiwa  kwa ndege ya PrecisionAir ikitokea Nairobi, Kenya inapounganisha safari hiyo inayoanzia Monrovia kupitia Accra, Ghana.

 Kocha huyo amesema hali ya hewa ya Dar es salaam haijatofautiana sana na hali ya hewa ya Liberia jana amekiri Dar es Salaam kuwa na joto kuzidi Monrovia

Msafara wa timu hiyo umetuwa na  watu 37,  wachezaji 21 na unaongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo Robert Alvin Sirleaf ambaye ni mtoto wa Rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, Samuel Sumo wakati Meneja wa timu ni Clarence Murvee. Daktari wa timu ni Samuel Massaquoi.

 Wachezaji waliomo kwenye kikosi hicho ni Abraham Andrew, Alfred Hargraves, Alpha Jalloh, Benjamin Gbamy, Cammue Tumamie, Erastu Wee, Ezekiel Doe, George Dauda, Hilton Varney, Ishmail Paasewe, Joekie Solo, Joseph Broh, Junior Barshall, Karleo Anderson, Mark Paye, Prince Jetoh, Prince Kennedy, Randy Dukuly, Raymond Blamonh na Winston Sayou.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...