Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, May 11, 2013

Rais Kikwete ahudhuria kikao cha SADC CAPE TOWN



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mkurugenzi Mtendaji na mratibu wa asasi ya Bill and Melinda Gates Foundation Bwana Mark Suzman jijini Cape Town Afrika ya Kusini.Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo Adam Malima.(picha na Freddy Maro)
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagana na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Misaada la Marekani USAID Dkt. Rajiv Shah muda mfupi baada ya kufanya naye mazungumzo katika ukumbi wa Cape Town Convention Centre jana
 Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akijadiliana jambo na Katibu mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Dkt.Tomaz Salomao mjini Cape Town Afrika ya Kusini leo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(Watatu kushoto) akiongoza kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalama  ya SADC kilichofanyika jijini Cape Town Afrika ya Kusini leo.Wengine katika picha ni wajumbe wa kamati hiyo akiwemo mwenyeji Rais Jackob Zuma wa Afrika ya Kusini(kulia),Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Namibia Bibi Netumbo Nandi-Ndaitwa(kushoto) na wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa SADC Dkt.Tomaz Salomao.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mwenyeji wake Rais Jackob Zuma wa Afrika ya Kusini wakitoka katika ukumbi wa hoteli ya Westin jijini Cape Town Afrika ya Kusini mara baada ya kumalizika kwa kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalma ya SADc kilichofanyika leo.Rais Kikwete alikuwa nchini Afrika ya Kusini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...