Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, May 30, 2013

Floyd Mayweather Jr KUPANDA ULINGONI September 14 NA Saul “Canelo” Alvarez

Floyd Mayweather Jr. (44-0, 26 KO’s) VS Saul “Canelo” Alvarez (42-0-1, 30 KO’s) step foot inside the ring on September 14th at the MGM Grand in Las Vegas, Nevada

Fainali ya Pool kufanyika Leaders Club, 'Safari Lager Higher Learning Competition 2013'


Meneja wa Bia ya Safari, Oscar Shelukindo akifafanua jambo kuhusu fainali za Pool 
Lwiza Mbutu akizungumza na waandishi wa habari. 
 Mchezaji wa Single wa Chuo cha CBE, Liliani Meori 
 Katibu wa Chama cha Pool Taifa (TAPA), Amos Kafwinga akizungumza wakati wa mkutano huo.
 Kiongozi wa bendi ya Twanga Pepeta, Lwiza Mbutu akionesha manjonjo yake wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo. Kushoto ni Rapa wa bendi hiyo, Jumainn Said.

Na Mwandishi Wetu

BENDI ya Muziki wa Dansi ya Twanga Pepeta, inatarajia kupamba fainali za Michuano ya mchezo wa Pool ngazi ya Taifa yajulikanayo kama 'Safari Lager Higher Learning Competition 2013'.
Fainali hizo zinatarajiwa kupigwa katika viwanja vya Leders kuanzia kesho mpaka Jumapili ambapo anatarajiwa kupatikana bingwa wa michuano hiyo iliyoanza kutimua vumbi Mei 5 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Meneja wa Bia ya Safari Lager ambao ni wadhamini wakuu wa shindano hilo, Oscar Shelukindo alisema, wameamua kuichukua bendi ya Twanga ili kutoa burudani wakati wa fainali hiyo ambayo pia itapabwa na nyama choma kutoka katika bar tano zilizoshinda katika shindano la nyama choma mwaka huu.

Shelukindo alisema, bingwa katika shindano hilo atajinyakulia kitita cha sh mil 2.5 pamoja na kombe huku zawadi nyingine zikitolewa kwa mshindi wa pili na mchezaji mmoja mmoja na kudai kuwa, timu nane zitachuano ambao ni mabingwa wa kila Mkoa.

Nae Kiongozi wa bendi ya Twanga Luiza Mbutu alisema, wamejipanga kufanya burudani kali ikiwa ni pamoja na kuwatambulisha wapenzi na mashabiki wao nyimbo mpya na kuwataka kuja kwa wingi kwani hakuna kiingilio.
Katika fainali hizo bingwa mtetezi ni chuo cha Sauti Mwanza ambacho pia kimefanikiwa kuingia katika kinyanyang’anyiro hicho mwaka huu.

Ashanti United haina mpango na 'Mafaza

'

Kikosi cha Ashanti kilichopanda Ligi Kuu









KLABU ya soka ya Ashanti United iliyorejea tena kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, imeweka bayana kuwa itafanya usajili wake kwa wachezaji vijana wenye uwezo kisoka badala ya kuwakimbilia 'mafaza' wakiwa na lengo la kutaka kuendelea kuzionyesha mfano klabu nyingine umuhimu wa kuzalisha 'jeshi' lao wenyewe.
Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mbaraka Hassani aliiambia MICHARAZO kwenye mazoezi ya timu hiyo uwanja wa Msimbazi, kwamba hawatawapapatikia mafaza kwa kuhofia kuja kujichanganya mbele ya safari ilihali wamejiwekea mikakati ya kutotaka kurudi walipotoka ambapo walisota kabla ya kurudia Ligi Kuu.
Mbaraka ambaye ndiye aliyeipandisha mwaka 2004 kabla ya kuzama msimu wa 2007-2008, alisema kutoa nafasi kwa vijana kutasaidia kuwatangaza wachezaji hao kama walivyofanya miaka ya nyuma na kuwaibua mastaa kadhaa  wanaotamba hivi sasa katika soka la Tanzania.
Baadhi ya nyotga hao ni pamoja na kipa wa kutumainiwa wa Yanga, Ally Mustafa Barthez, Jabir Aziz, Juma Jabu, Mohammed Kijuso, Juma Nyosso, Deo Ngassa na wengineo.
"Hatujaanza rasmi kufanya usajili, lakini tukianza tutajikita kwa vijana zaidi kwa lengo la kuwapa nao nafasi ya kuonwa, si unajua Ashanti ni kama chuo kazi yetu kuzalisha wengine wachukue ndivyo tutakavyofanya hata safari hii kwa vile tumepania kuonyesha mfano kwa klabu nyingine," alisema Mbaraka.
Mbaraka, alisema anaamini kuwapa nafasi vijana kunasaidia kukuza soka la Tanzania kuliko kuendelea sera ya kung'ang'ania wachezajki wenye majina ambao mara nyinbgi usumbua hasa kwenye suala la masilahi ikizingatiwa klabu yao haina wafadhili zaidi ya wanachama na wadau wake kuchangishana fedha kuiendesha.
Ashanti imerejea ligi kuu msimu ujao pamoja na klabu za Rhino Rangers ya Tabora na Mbeya City na wanaendelea kupima wachezaji kwa ajili ya kupata itakaowasajili.

KASEBA APANIA KUMKALISHA MMALAWI


Na Elizabeth John


BONDIA wa ngumi za mateke ‘Kick Boxer’ Japhet Kaseba amesema amejipanga kuweka rekodi nzuri katika tasnia hiyo kwa kumchapa Mmalawi, Rasco Chimwanza katika pambano lao la kuwania ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati linalotarajiwa kuchezwa Juni 8, mwaka huu.



Akizngumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Kaseba alisema anajua kama bondia huyo ni nyota katika tasnia hiyo, lakini kutokana na maandalizi aliyoyapata atahakikisha anaweka heshima katika ngumi za mateke.
“Namshukuru mungu nina afya nzuri hadi sasa na naendelea na mazoezi kwajili ya pambano hilo naomba Watanzania wajitokeze kwa wingi katika ukumbi huo wa DDC Magomeni,” alisema Kaseba.
Naye Katibu Mkuu wa Oganizasheni ya ngumi ya za kulipwa Tanzania (TPBO), Ibrahim Kamwe alisema maandalizi ya pambano hilo yamekamilika, na tayari wamemtumia nauli Mmalawi huyo na kwamba anategemea kuingia nchini Juni 5.
Alisema TPBO imemtengenezea mazingira mazuri ya ushindani, Kaseba na kwamba wanategemea atafanya vizuri katika pambano hilo kutokana na maandalizi ambayo anaendelea kufanya.

 Nae kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake kukiwa na clips za mabondia  wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali

CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata DVD hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo

Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia
 
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
hizo ni ya Kalama Nyilawila ,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na
Francis  Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe. 
 
 mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

MTOTO RAMLA ADAM ASHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA

MTOTO RAMLA ADAM
MTOTO RAMLA ADAM kushoto akilishana keke na Zainabu Mhamila 'Ikota' wakati wa siku yake ya kuzaliwa kwake iliyofanyika nyumban kwao Buguruni ramla alitimiza miaka sita katika siku yake hiyo
Mtoto Ramla Adam kulia akiwa katika picha ya pamoja na mama yake mzazi na Zainabu Mhamila 'Ikota'

Wednesday, May 29, 2013

BEN PAUL KUWASINDIKIZA MISS UN-COLLEGE TEMEKE


 Florence Josephat, mratibu Redd's Miss Uni-college. Kulia ni mmoja wa waratibu Francisca Mansilo.


MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Bernard Paul ‘Ben Paul’, anatarajiwa kuwasindikiza warembo wa kinyang’anyiro cha Redd’s Miss Uni-college Temeke kitakachofanyika kesho katika ukumbi wa Club Bilicanas, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, mratibu wa shindano hilo, Florence Josephat, alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika na kwamba kilichobaki ni shoo yenyewe ambayo alitamba itakuwa katika ubora wa hali ya juu.
Alisema kuwa jumla ya warembo 13 wanatarajia kupanda jukwaani siku hiyo, ikiwa ni baada ya kunolewa vilivyo kwa takribani wiki tatu na kwamba wameiva kuwapagawisha watakaofika kushuhudia uhondo huo.
“Maandalizi yote yamekamilika hivyo tunawaomba wapenzi wa burudani na urembo kwa ujumla kujitokeza kwa wingi siku hiyo kwani kipenzi cha warembo, Ben Paul, atatoa burudani ya hali ya juu itakayoambatana na shoo kutoka kwa warembo wetu kutoka vyuo vitano vilivyopo Temeke,” alisema.
Alivitaja baadhi ya vyuo hivyo kuwa ni Chuo Kikuu cha Uganda, TIA, Chuo cha Bandari, DUCE na Chuo cha Utalii, huku akitamba kuwa kutokana na ubora wa warembo walionao, wana imani mwaka huu Redd’s Miss Tanzania atatoka katika kitongoji chao hicho.
Florence ambaye alikuwa mshiriki wa fainali za Miss Tanzania 2008, aliwataka wapenzi wa urembo na burudani, hasa wanafunzi wa sekondari na vyuo, kujitokeza kwa wingi siku ya shoo yao ili kujionea warembo bomba, huku wakipata burudani ya aina yake.
Alitaja kiingilio cha shoo yao kuwa ni Sh 10,000 na kwamba mbali ya kinywaji cha Redd’s ambao ndio wadhamini wakuu wa mashindano hayo, wadhamini wengine ni Shome Decoration & Catering, djfetty.blogspot.com na Lamada Hotel.

Odama aisambaza ‘Whitch Doctor’


Na Elizabeth John


MWANADADA ambaye anafanya vizuri katika tasnia ya filamu nchini, Odama amesambaza filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Whitch Doctor’.
Akizungumza Dar es Salaam, nyota huyo alisema filamu hiyo ameisambaza hivi karibuni anaomba wadau wa kazio zake wakae mkao wa kula kwaajili ya kupokea vitu vizuri kutoka kwake.
“Namshuku mungu asilimia kubwa ya kazi zangu zinapokelewa vizuri na mashabiki wangu hivyo ninaimani hata kazi hii itapokelewa vizuri kutokana na ubora uliopo ndani yake,” alisema Odama.

MISS SINZA/ MISS TANZANIA 2012-2013 BRIGIT ALFRED AWAFUNDA WAREMBO WA REDD'S MISS SINZA 2013


 Miss Sinza na Miss Tanzania 2012-2013, Brigit Alfred (kulia) akizungumza na Warembo wanaotarajia kuwania Taji la Redd's Miss Sinza 2013, wakati alipowatembelea katika Kambi yao ya mazoezi jana katika Ukumbi wa Meeda Sinza na kuwafunda kuhusu mashindano hayo kuelekea shindano hilo linalotarajia kufanyika Juni 7 mwaka huu kwenye Ukumbi huo. Katika shindano hilo Viingilio vitakuwa ni Sh. 20,000 kwa VIP na viti vya kawaida ni Sh. 10,000. Shindano hilo limedhaminiwa na Mtandao wa www.sufianimafoto.com, kinywaji cha Dodoma Wine, Chilly Willy Energy Drink, Clouds Media Group, CXC Africa, Saluti5 na Fredito Entertainment.
 Miss Sinza na Miss Tanzania 2012-2013, Brigit Alfred (katikati) akipozi na warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Sinza 2013, wakati alipowatembelea kwenye Kambi yao ya mazoezi katika Ukumbi wa Meeda Sinza.
Miss Sinza na Miss Tanzania 2012-2013, Brigit Alfred (katikati) akipozi na warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Sinza 2013, wakati alipowatembelea kwenye Kambi yao ya mazoezi katika Ukumbi wa Meeda Sinza. Picha zote na www.sufianimafoto.com

The Finest’ ya Mwana FA yapisha msiba wa Ngwea


Na Elizabeth John

MKALI wa muziki wa bongo fleva nchini, Mwana FA amesema ameahirisha kufanya shoo yake ambayo inajulikana kwa jina la ‘The finest’ ambayo ilitakiwa kufanyika leo, ili kuupisha msiba wa msanii wa hip hop nchini, Albert Mangwea uliotokea Mei 28 mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwana FA alisema ameamua kufanya hivyo kutokana na umuhimu wa msanii huyo katika tasnia ya muziki wa hip hop nchini.
Mbali na Mwana FA, wasanii wengine ambao wamesogeza mbele na kuhairisha kufanya shoo zao ni pamoja na Lady Jay Dee, Izzo Business, Joeh Makini na Kalapina.

SUPER NYAMWELA AKAMILISHANYIMBO YAKE MPYA YA DUVELLEE DUVELLEE LA POP BONGO


MNENGUAJI Mahiri wa muziki wa dansi nchini, anayeshambulia na bendi ya Extra Bongo, Super Nyamwela, amekamilisha Song lake jipya linalokwenda kwa jina la Dullee Duvellee, linalopigwa katika mtindo wa Bongo Pop.

Akizungumza na mtandao huu wa www.sufianimafoto.com, Nyamwela, amesema kuwa Wimbo huo aliourekodia katika Studio za C91, zilizopo Kinondoni, amemshirikisha Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Muki kutoka katika Kundi la Makomandoo lililo chini ya THT.

Aidha alisema kuwa Msanii huyo aliyemshiriki ni yule anayetamba na Song lake kali ya Staili ya Kibega, ambao kwa pamoja katika wimbo huo wemefanya kazi ya kueleweka na inayomvutia kila mmoja atakayepata bahati ya kuusikiliza wimbo huo.

''Hivi sasa najipanga kuzindua staili yangu mpya ya Bongo Pop, inayokwenda na 'Swaga za Duvellee Duvellee' ambyo kwa maana halisi ya kiswahili cha Kitaa ni Shwari Shwari, na tayari wimbo huu nimeshausambaza katika Vituo mbalimbali vya Redio nchini na baadhi wameshaanza kuutendea haki kwa kuupiga na kuwapa raha wasikilizaji''. alisema Nyamwela

Pia Nyamwela amesema kuwa yupa katika maandalizi ya kurekodi Video ya Wimbo huo mwishoni mwa wiki hii katika Studio mpya za THT.http://www.sufianimafoto.com/

MASHINDANO YA CHESS KUTIMUA VUMBI JUNI 14-6


 Mkurugenzi wa Spicenet Tanzania, Viney Choundary akizungumza  na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mashindano ya wazi ya kimataifa yajulikanayo kama ‘Spicenet Tanzania Open Chess Championship 2013’ yanayotarajiwa kutimua vumbi juni 14-16 katika  ukumbi wa Meru uliopo katika jengo la Golden Jubilee Tower mtaa wa Ohio jijini Dar es Salaam. Kulia ni Emmanuel Mwaisumbe na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha mchezo wa Chess, Joe Anea.
Emmanuel Mwaisumbe akifafanua jambo.

Na Elizabeth John
CHAMA cha Mchezo wa Chess nchini, kimeandaa mashindano ya wazi ya kimataifa yajulikanayo kama ‘Spicenet Tanzania Open Chess Championship 2013’ ambayo yanatarajia kuanza kutimua vumbi Juni 14 hadi 16 katika ukumbi wa Meru uliopo katika jengo la Golden Jubilee Tower mtaa wa Ohio jijini Dar es Salaam
Katika kunogesha mashindano hayo ambayo yataweka rekodi Afrika Mashariki, yatashirikishwa na bingwa ambaye alikua ni mchezaji namba tatu duniani mwaka 1990, Nigel Short.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Chess, Joe Anea alisema mashindano hayo yatahusisha wachezaji kutoka Tanzania, Zambia, Uganda na Kenya na kwamba yanatarajiwa kuhudhulia na jumla ya wachezaji 80, huku wachezaji 50 wakitoka Tanzania na 30 kutoka nchi za jirani.
Alisema kuwa mshindi wa kwanza atajinyakulia sh. 1,000,000, sh.500,000 kwa mshindi wa pili, sh. 300,000 kwa mshindi wa tatu, sh. 100,000 kwa mshindi wa nne na tano.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kampuni ya Spicenet, ambayo ndio wadhamini wa mchezo huo, Vinay Choudary alisema wameamua kuungabnisha nguvu na chama cha Chess kuufufua mchezo huo Tanzania katika jitihada za kuhakikisha nchi yetu inang’ara katika medani ya michezo katika mashindano ya kimataifa.
“Nia yetu ni kukisaidia chama hiki kuhakikisha mchezo huo unatangazwa na hatimaye kutambulishwa kwa watu wengi kupitia shule, taasisi, vyuo vikuu na njia nyingine,” alisema.
Naye Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Benson Chacha aliupongeza uongozi wa Chess pamoja na wadhamini wake kwa kuamua kuurudisha mchezo huo ambao ulisajiliwa na BMT mwaka 1984.
“Sisi kama Baraza tutausaidia mchezo huu kupata vitambulisho mbalimbali vya kushiriki mashindano ya mchezo huu, pia tunaomba wadau wajitokeze kudhamini kwa lengo la kukuza michezo nchini,” alisema.

Familia ya Ngwair watoa taarifa ya mazishi na jinsi mwili utakavyoletwa Bongo


http://3.bp.blogspot.com/-WhLAsO1Z0Cg/TftKo0GeYeI/AAAAAAAAAkY/Z6SKc0_7gz0/s1600/NgweaWEB.jpg
Ngwair enzi za uhai wake
BABA Mdogo wa 'Membaz' wa kundi la Chember Squad, Albert Mangwea 'Ngwair', Mzee Mangweha ambaye yuko Mbinga Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangweha ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam Mbezi Beach. 
  

Baba huyo mdogo alisema kuwa kesho ndo watarudi Dar es Salaam pamoja na kaka yake yaani baba mkubwa wa marehemu. 
 
Kuhusu mwili kuletwa hapa Tanzania kutoka Afrika Kusini baba mdogo amesema kuwa mpaka sasa hawajajua jinsi gani mwili huo utafika hapa lakini kuna ndugu zao ambao tayari washaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na ubalozi wa Afrika Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa.

Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote watakapowasili kesho baba mdogo na baba mkubwa baada ya kikao cha familia watatoa taarifa.
Lakini asuibuhi mmoja wa ndugu wa marehemu kutoka mkoa wa Mara alisema kuwa mwili wa msanii huyo aliyekuwa mkali wa Hip hop utakapowasili nchini utazikwa mjini Morogoro ambapo tayari kuna msiba umewekwa na mama yake.
Ndugu huyo alikuwa akihojiwa moja kwa moja na kituo kimoja cha redio na kusema wana ndugu wamekubaliana Ngwair akazikwe Morogoro alipohifadhiwa baba yake.
Ngwair, aliyefahamika baada ya kutoa kibao cha Ghetto Langu mwaka 2003 kabla ya kupakua albamu ya Mimi na kisha kufuatiwa na Nge, alifariki jana nchini Afrika Kusini kwa kile kilichoelezwa kujidunga dawa za kulevya, ingawa bado haijathibitishwa kidaktari alipoenda kufanya shoo na msanii mwenzake M2P. 

WASIFU WA MAREHEMU NGWAIR


 MAREHEMU Albert Kenneth Mangwea alizaliwa Novemba 16, 1982 mjini Mbeya akiwa ni mtoto wa mwisho kati ya watoto 10 wa baba yake na wa sita kwa mama.
Kiasili Ngwair alikuwa mwenyeji wa mkoa wa Ruvuma kabila la Kingoni, ingawa amekuwa mjini Morogoro na mkoa wa Dodoma.
Shule ya Msingi aliisoma Shule ya Bungo mjini Morogoro alikohamia akiwa na miaka mitano kabla ya kuhamia Dodoma kulamizia darasa la saba toka la tano alilohama nalo Shule ya Mlimwa.
Sekondari aliisoma Mazengo Sec kabla ya kuendelea Chuo cha Ufundi cha Mazengo pia mjini Dodoma alipoanza kujihusisha na muziki kabla ya kutua kundi la Chamber Squad lililoundwa na Jafarah, Jay Mo, Noorah, Mez B, Mchizi Mox na Dark Master.
Amewahi kunyakua tuzo ya Kili Music Award kupitia kipengele cha muziki bora wa Hiphop, huku nyimbo kadhaa zilimtambulisha vyema kwa mashabiki baadhi ikiwa ni  Ghetto Langu, Mikasi na nyingine za kushirikishwa na wasanii mbalimbali.
Katika maisha yake ya muziki aliwahi kutoa albamu mbili za Mimi ya mwaka 2005 na Nge ya mwaka juzi ambayo hata hivyo haikufanya vyema sokoni kama ile ya awali.

Monday, May 27, 2013

KING CLASS MAWE KUPAMBANA NA BAUNSA JUNI 16 PANANDI PANANDI ILALA


KING CLASS MAWE
BAADA ya kumsambalatisha Amosi Mwamakula kwa point  bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' anakabiliwa na kibarua kizito kwa kupanda ulingoni na bondia  Patrick Anthony Kavako 'Baunsa' wa Morogoro  mpambano wa raundi 8 utakaofanyika katika ukumbi wa Panandi panandi Ilala Bungoni Juni 16 akizungumzia mpambano huo kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' alisema kuwa mpambano huo ni wa kukata na shoka ambao si wa kukosa kwani kila mmoja amejitahalisha kivyake hivyo wasubili tu siku ya mpambano huo
Patrick  Kavako'Baunsa'
Unajua morogoro na Dar es salaam ni mahasimu katika michezo yote ukiangalia na sasa wamekutanishwa vijana katika masumbwi hivyo kila mmoja anaitaji ushindi ili ajiongezee rekodi yake kwani 'King Class Mawe' ato kubali kupigwa na Kavako ato kubali kabisa kupoteza mpambano wake kiraisi kwani na yeye anaitaji ajulikane katika ulimwengu wa masumbwi na kuiperekea sifa morogoro kama ilivyo kwa mabondia wengine wanao tamba mkoani hapo 
Mpambano huo ulioratibiwa na Kinyogoli Fondition kwa kushlikiana na PST itakuwa chachu kwa vijana kuendelea kuupenda na kuucheza mchezo huo unaopendwa na wengi nchini
mbali ya mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ya kukata na shoka bondia Abuu Mtambwe ataoneshana umwamba na Kassim Gamboo na Bondia mkongwe kabisa Yohana Robart atamenyana na Mussa Sunga
 
Kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini,Rajabu Mhamila ‘Super D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake kukiwa na clips za mabondia  wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali

CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata DVD hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo

Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia
 
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
hizo ni ya Kalama Nyilawila ,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na
Francis  Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe. 
 
 mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

Zantel yazindua Epiq Open Mic



Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond na Ney wa Mitego wakitumbuiza jukwaani kwenye uzinduzi wa tamasha la  Epiq Open  Mic 
=======  ======  ========
Katika kuelekea msimu wa sita wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star  Search, kampuni ya simu za mikononi ya Zantel leo imezindua Epiq Open  Mic ikiwa ni nafasi nyingine kwa vijana wenye vipaji vya muziki kuonyesha  vipaji vyao kabla usaili wa Epiq Bongo Star Serach haujaanza.

Epiq  Open  Mic  inatarajiwa  kuwapa  nafasi  vijana  kujifunza  misingi  ya  muziki kutoka kwa mmoja wa watayarishaji wa muziki maarufu zaidi nchini,  Marco Chali. Marco  Chali  ambaye  pia  ni  mtunzi  na  mwimbaji,  ametayarisha  nyimbo  nyngi ambazo zimeshinda tuzo ndani na nje ya nchi za wasanii kama Ms. 

Trinity  kutokea  Jamaica,  A.Y  wa  Tanzania,  Prezzo  wa  Kenya,  J  Martins  kutoka Nigeria na wengine wengi. Tamasha  hilo  la  Epiq  Open  Mic,  ambalo  ni  la  bure  litazinduliwa  rasmi  kwenye  viwanja  vya  Mwembe  Yanga  Temeke  tarehe  26  ya  mwezi  huu  ikisindikizwa  na  wakali  kibao  wa  Bongo  flavor  kama  Diamond  Platnumz,  Madee, Godzila, Ney wa Mitego, Mabeste na Mrap.

Akizungumza  wakati  wa  kuzindua  matamasha  hayo,  Afsa  Biashara  Mkuu wa Zantel, Sajid Khan alisema kampuni ya Zantel inaaminini katika  kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao. ‘Muziki ni ajira kwa vijana wengi, na kuamini hilo ndio maana kampuni ya  Zantel  imeamua  kuwafikia  vijana  wote  wenye  vipaji  na  kuwapa  nafasi  ya  kuonekana’ alisema Khan.

Baada  ya  uzinduzi  wa  tamasha  la  Epiq  Open  Mic  Mwembe  Yanga  tamasha  hilo  litaendelea  kila  jumamosi  kwenye  makao  makuu  ya  Zantel  likiwapa nafasi vijana kujisajili na kurekod sauti zao.  Vijana watakaorekodi sauti zao watapigiwa simu na timu ya watayarishaji  wa muziki chini ya Marco Chali pamoja na wanamuziki ili kuwapa ushauri   wa namna ya kuboresha muziki wao zaidi. 

‘Zantel imejipanga kutumia fursa hii kuwahamasisha vijana kushiriki katika  kukuza  vipaji  vyao,  kuongeza  uelewa  wa  mambo  ya  muziki  pamoja  na  kuchangamkia fursa zilizopo katika muziki’ alisisitiza Khan. Epiq  Open  Mic  pia  inatarajia  kuwapa  fursa  ya  kurekodi  baadhi  ya  vijana  watakaokua na vipaji.

GARI LAGONGA TRENI DAR MKE ALIYEKUWA AKINDESHA YUPO TAABANI MUME WAKE AFA PAPO HAPO


Wakazi wa Dar es Salaam wakingalia eneo ajali hiyo ilipotokea majira ya asubuhi leo.
 
Treni likiendelea na huduma zake likipita jirani na eneo lilipogongana na gari dogo aina Honda CRV jirani na Moshi Bar Dar es Salaam asubuhi leo. Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa ni mume wa dereva wa gari hilo alifariki papo kwa hapo. Mwanafunzi wa shule aliyejulikana kwa jina la Grace Samsoni alipata michubuko  wakati wa ajali hiyo alitibiwa na kuruhusiwa katika hospitali ya Amana.
 
Baadhi ya wakazi wa eneo la Moshi Bar karibu na Mombasa nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakiangalia kioo cha gari aina ya Honda CRV eneo ajali ilipotokea. 

Agnes Msoka aliyekuwa akiendesha gari lililogonga treni na kusababisha kifo akisubiri kufanyiwa upasuaji hospitalini.
 
Dereva wa gari liligonga Treni akiwa amelazwa ICU kwa matibabu.

Gari iliyogonga treni likiwa limeegeshwa Kituo cha Polisi Kikuu cha TAZARA Dar es Salaam.

Huyo ndo marehemu aliyefariki katika ajali hiyo.

HAMADUU MWALIMU ALIVYO MWONESHA UBABE COSMAS KIBUGA


Bondia Cosmas Kibuga kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Hamaduu Mwalim wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki mwalimu alishinda kwa pointi  picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Cosmas Kibuga kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Hamaduu Mwalim wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki mwalimu alishinda kwa pointi  picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Cosmas Kibuga akimsubili kwa hamu hamaduu mwalim baada ya kudondoka chini wakati wa mchezo wao jana
Bondia Hamaduu Mwalimu kushoto akioneshana umairi wa kurushiana makonde na Cosmas Kibuga wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana Mwalimu alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mpambano wa utangulizi kwa ajili ya kusafisha uwanja

WASANII WAKABIDHI PICHA YA KUCHORA YA RAIS JAKAYA KIKWETE


 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam akipokea picha ya Rais Jakaya Kikwete iliyochorwa na wasanii wa Kikundi cha Manuari Dar es Salaam kwenye tamasha na mastaa chipukizi lililofanyika juzi Dar es Salaam
Msanii Salum Hamisi wa Kikundi cha Safi Culture Group akicheza kusimama na mkono mmoja katika tamasha la wasanii chipukizi jana Dar es Salaam.

Kichanga cha siku nne chaokotwa shimoni alikokaa kwa siku 6




UKISHANGAA ya Mussa basi utayaona ya Firauni, usemi huu umethibitika Songea baada ya Mtoto Bahati Upendo mwenye siku 3 toka azaliwe aliyekuwa amewekwa kwenye mfuko wa mbolea kisha kutupwa kwenye shimo kuokolea akiwa hai licha ya kuishi shimoni humo kwa sita sita.
 
Ndani ya shimo hilo amekaa siku 6 bila kula wala kunywa hadi alipo okotwa na wasamaria wema...
Hivi sasa yuko Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma akiwa Salama  Salimini .
Yeyote Mwenye nafasi ya kumsaidia mtoto huyu anaweza kwenda moja kwa moja Hospitali au wasiliana na namba zifuatayo,  mchango  utafuatwa 0755061588 au 0755 731 234.
Dawati la Police Wanawake Mkoa wa Ruvuma wakiwa na Wauguzi kuangalia usalama wa Mtoto huyo aliye Tupwa. Kutoka kulia ni Muguzi Rukia Twahili anaye fuata Devota Umbela na aliye mshika mtoto Mwenyekiti wa Mtandao wa Police Wanawake Fadhila Chacha na wa mwisho kushoto ni A nna Chaima

USAHIRI WA SHINDANO LA BIBI BOMBA WAFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA LEADERS CLUB, TAMASHA LA NYIMBO ZA MAKABILA LINAENDELEA


Mshiriki wa shindano la Bibi Bomba, Bi. Veronica Kayombo (katikati) akionesha umahiri wa kuimba nyimbo wakati wa mchujo wa kuwatafuta washiriki 10 watakaoingia katika nyumba kwa ajili ya shindano hilo lililoandaliwa na Clouds Tv na kudhaminiwa na Airtel. Kushoto ni Anna Nicolous na Rozalia Marko
 Majaji wa Shindano la 'Bibi Bomba' kutoka (kushoto) Zamaradi Mketema, Babuu wa Kitaa, Regina Mwalekwa na Benny Kinyaiya, wakifuatilia washiriki wakati wakijieleza kuhusu ufahamu wa shindano hilo, lililoanza leo katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, wakati wa Tamasha la Nyimbo za Makabila 'Tamadunika' linaloendelea hivi sasa viwanjani hapa.
 Mmoja kati wa washiriki 32, akijieleza wakati wa mahojiano rasmi viwanjani hapo....
  Mmoja kati wa washiriki 32, akijieleza wakati wa mahojiano rasmi viwanjani hapo....
 Baadhi ya wanacrew wasimamizi wa shoo hiyo, wakiwa eneo la tukio.....
 Babu wa Kitaa, (kushoto) akiburudika kwa miondoko ya sebene na mmoja wa washiriki wa shindano hilo.
 Sehemu ya washiriki waliojitokeza kushiriki shidano hilo...
 Mshiriki akijieleza......
 Watazamaji wakifuatilia shindano hilo......
Waongozaji wa Tamasha hilo, wasema lolote, Mbwiga Mbwiguke na Suzzy Bartazar, wakijiandaa kusherehesha Tamasha hilo la Nyimbo za Makabila.
 Benny Kinyaiya, akitoa maelezo mafupi kwa washiriki wa shindano la Bibi Bomba.......
 Gea Habib, akifafanua jambo kwa washiriki wa shindano hilo....
 Sehemu ya watazamaji......
Sehemu ya watazamaji waliojitokeza kushuhudia Tamasha hilo.....
Picha na www.sufianimafoto.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...