Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, July 22, 2012

Michango ya Maafa MV Skagit Yaanza Kupokelewa



Afisa Muandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Tanzania Nd. Juma Kimtu akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Mchango wa Maafa wa Shilingi 10,000,000/- hapo ofisini kwake Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Nyuma yake ni Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea mchango wa Maafa wa shilingi 10,000,000/- kutoka kwa Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than hapo katika Ofisi yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Na Othman Khamis Ame

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewanasihi Wananchi kuendelea kuiamini Serikali katika kupokea Taarifa zake hasa wakati wa kutokea Majanga na Maafa.
 Nasaha hizo amezito hapo katika Ofisini yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar wakati akipokewa mkono wa Pole kutoka kwa Taasisi mbali mbali za Umma na Kijamii. 
Salamu hizo za mkono wa pole zimetolewa kwa Balozi Seif na Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } na ule wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii ya Tanzania { NSSF } ambapo kila moja ilikabidhi mchango wa Shilingi Milioni kumi { 1,000,000/- }.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...