Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, July 21, 2012

TAMASHA KUBWA LA KUWAAGA IMUKA SINGERS KUFANYIKA DIAMOND JUBILEE JULAI 22


 Mratibu wa Tamasha la Imuka, Harris Kapiga akifafanua jambo wakati wa mkutano waandishi wa habari Dar es Salaamleo kuhusu tamasha la Imuka litakalofanyika Jumapili Julai 22 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. Kushoto ni Katibu wa Gospel House of Talent, Charles Gao na Mkurugenzi wa Imuka Singer Cosad-Tanzania, Smart Baitan.
Wasanii wa Imuka Singers wakionyesha umahiri wa kucheza ngoma wakati wa mkutano wa kuwatambulisha kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu

Gospel House of Talent kwa kushirikiana na Cosad-Tanzania, wanakuletea tamasha kubwa kwa ajili ya kuwaaga imuka singers walioalikwa kwenda marekani september mwaka huu.
 Imuka Singers kutoka bukoba watasindikizwa na Cristina Shusho, Upendo Nkone, The Voice, Jane Misso, Injilist Kijitonyama, Madame Ruth  na Chris, Martha Mwaipaja , DP, Brother Joshua Mlela na Bahati Bukuku.
kiingilio wakubwa sh 10,000 na watoto sh 3,000.tiket zinapatikana mlangoni siku hiyo ya tamasha tar 22/7/2012 na pia kiingilio chako kitasaidia nauli ya kwenda marekani kwa kikundi hiki kutoka bukoba.
tamasha hilo litafanyika siku ya tarehe 22/7/2012 jumapili hii kuanzia saa saba mchana pale diamond jubilee vip hall
wageni maalumu ni waziri wa maliasili na utalii balozi hamis kagasheki na mkuu wa mkoa wa kagera ,kanal mstaafu fabiani masawe,
njoo uone Imuka Singers watakachokifanya marekani kuitangaza Tanzania.
kwa mawasiliano zaidi piga simu no 0767 93 37 37 au 0712 70 39 86.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...