Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, November 2, 2012

TAMASHA LA MITIKISIKO YA PWANI DAR LIVE TAR 3-11-2012



Tamasha la Mitikisiko ya Pwani lilianza mwaka 2004 katika ukumbi wa Traventine, mwaka 2008 lilifanyika Msasani club, mwaka 2009 likafanyika P.T.A. Hall iliyoko ndani ya viwanja vya Mwalimu Nyerere  Kilwa road, mwaka 2010 likafanyika Diamond Jubilee Hall na mwaka 2011 likafanyika tena P.T.A. Hall.
Mwaka huu 2012, tamasha la Mitikisiko ya Pwani linafanyika ukumbi wa Dar Live tarehe 3/11/2012 siku ya Jumamosi. Tamasha litafungua milango saa nne asubuhi. Awamu hii itakuwa ni kwa watoto na watu wazima ambao ambao wako mbali na jiji au wale ambao hawana rukhsa kutembea usiku. Na kiingilio kwa awamu hii  ni  shilingi 5,000/= kwa wakubwa na watoto  shilingi 3,000/=, watapata burudani kutoka katika kundi maarufu la Wanne Star.
Awamu ya pili itaanza saa mbili usiku hadi majogoo kwa kiingilio cha shilingi 10,000 tu. Awamu hii itapata burudani kutoka kwa bendi zipatazo 13 za taarab ambazo ni Diamond Taarab Kutoka Zanzibar, Manuari, T.Moto, Zanzibar Njema, New Zanzibar Modern Taarab, Kings Modern, East Africa Melody, Dar Modern Taarab, Coast Modern Taarab, Five Star Modern Taarab, Jahazi Modern, Mashauzi Classic na Bibie Khadija Kopa, 
WAUTAKAAA! KIAFRIKA ZAIDI….!

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...