Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, February 2, 2014

Hatimaye Babi apumua, familia yake yamfuata Malaysia


Babi na mkewe Mariam Abdulkadir waki-show Super Market nchini Malaysia baada ya mkewe huyo kutua na watoto wao
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Malaysia katika klabu ya Ligi Kuu ya UiTM, Abdi Kassim 'Babi' amepumua baada ya familia yake kutoka visiwani Zanzibar kuwasili nchini Malaysia.
Akizungumza na MICHARAZO  kutoka Malaysia, Babi alisema familia yake ikiongozwa na mkewe, Mariam Abdulkadir iliwasili wikiendi hii ikiwa na mkewe Mariam Abdulkadri aliyeambatana na watoto wake.
Babi alisema kutua kwa familia yake kwa ajili ya kuishi nayo nchini Malaysia wakati akitumikia mkataba wake wa mwaka mmoja UiTM imempa faraja kubwa kwani alikuwa hana amani alipokuwa mbali na familia hiyo.
"Kwa kweli nimefurahi na kufarijika kuwasili kwa familia yangu nchini hapa, sikuwa na amani na pengine sasa nitacheza maradufu kuisaidia timu yangu kuliko ilivyokuwa siku za nyuma familia ikiwa Zanzibar," alisema Babi.
Babi anayetarajiwa kushuka tena dimbani na klabu yake katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Ijumaa hii, baada ya kuiongoza mechi mbili zilizopita kwa kushinda dhidi ya Kuala Lumpur na nyingine kupata sare ya 1-1 dhidi ya Johor, bao la timu yake akilifunga yeye.
Kiungo huyo nahodha wa zamani wa Yanga, amesajiliwa UiTM akitokea KMKM ya Zanzibar iliyomnyakua msimu huu baada ya kuachana na Azam aliyokuwa akiichezea kwa mkataba wa misimu miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...