Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, November 16, 2012

SUMATRA KUWAKAMATA WATAKAOPANDISHA NAULI ZA MABASI




DAR ES SALAAMJ, Tanzania
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imesema itawakamata wamiliki wa magari wote watakaohusika katika kupandisha nauli hovyo hvyo.
Msemaji wa Mamlaka hiyo, David Mziray amesema hayo jijini Dar es Salaam leo wakati alipokuwa akizungumzia taarifa kuwa kuna baadhi ya madereva na makondakta kupandisha nauli kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.
Alisema wamejipanga vizuri kwani wamewaandaa vijana watakaoshirikiana na Jeshi la Polisi ili kuzikamata kampuni za mabasi ambazo zitabainika kupandisha nauli kinyume cha sheria.
 Mziray alisema katika kipindi hiki wataendesha opresheni kila siku ya kukamata kampuni ambazo zitaenda kinyume na mkataba wao wa  leseni, itatozwa fani ya  sh 25000.
Sambamba na hilo, aliwatahadhalisha wamiliki wa magari hayo kuwa makini ili kuepuka kutozwa faini ambazo kwa kiasi kikubwa zinaumiza wao na wala siyo madereva na makondakta.
“Nafahamu kweli kuna baadhi ya magari hivi sasa yamekwishaanza kupandisha nauli kutokana na kuongezeka kwa abiria wanaosafiri kwenda kuungana na familia zao katika kipindi cha kusherehekea Sikukuu ya X-mas”alisema.
Mziray alisema SUMATRA haitasita kuzifutia leseni kampuni ambazo zitaonekana kuwa sugu katika kujiingiza kwenye vitendo hivyo vya kupandisha nauli kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwaibia wananchi.
Vile vile aliwaasa abiria  kutoa ushirikiano katika operesheni hiyo ya kuzikamata kampuni zinazojihusisha na upandishaji huo wa nauli, wakati mwingine wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na abiria wenyewe kuwa wagumu kuwafichua madereva na makondakta wanaofanya hivyo.
Hata hivyo,  Mziray alitoa wito kwa wananchi kupanga nasafari zao kwa utaratibu na wala siyo kurupuka kwani mara nyingi wale wanao kurupuka kwa kutaka kusafiri siku hiyo hiyo ndiyo maranyingi wanaokumbana na ubabaishaji huo katika kupata tiketi.

4 comments:

  1. Aw, this was an eхceptiοnally nice pоst.

    Tаking a few minutes and actual effort to maκe a top notсh article?

    but what can I say? I hesitate a whole lot and never manаgе to get anythіng done.

    http://www.facebook.com/hgcinеmatic
    Here is my page ; Wedding

    ReplyDelete
  2. Nice resρonse in retuгn of thiѕ question with firm аrgumentѕ and еxplaining еverythіng abοut
    that.http://bethеl.patch.сom/еvеntѕ/the-ultimatе-fightеr-ѕeаѕоn-16-еpiѕode-11-fight-the-perfect-fight-watch-it-for-frеe-onlinе-ѕtream
    Also visit my webpage The Ultimate Fighter Season 16 Episode 11 Free Stream

    ReplyDelete
  3. Thiѕ іѕ very іnteгesting, You're a very skilled blogger. I have joined your rss feed and look forward to seeking more of your wonderful post. Also, I'vе shareԁ your web sіte
    in my ѕoсial nеtωоrks!
    httρ://blogs.reԁіff.com/vannіаlford2590/2013/01/06/underemрloyeԁ-sеaѕon-1-episoԁe-11-thе-meѕsage-ωаtch-free-online-ѕtrеam/
    Review my web blog Underemployed Season 1 Episode 11

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...