Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, July 2, 2012




Miaka kumi tangu kupotea kwa bia iliyopata umaarufu na heshima kubwa miaka  ya 2010 kurudi nyuma maarufu kama KIBO GOLD BIA, Kampuni ya bia ya Serengeti iliyokuwa ikizalisha bia hiyo, imezindua tena bia hiyo na kuingiza sokoni tayari kutumika kama vinywaji vingine vinavyozalishwa na kampuni hiyo.


Akizungumza na wageni waalikwa na waandishi wa habari waliohudhuria katika uzinduzi huo uliofanyika katika kiwanda cha Serengeti tawi la moshi mkoani Kilimanjaro, Meneja wa bia ya Serengeti bw. Alln Chonjo , amesema kampuni hiyo merefu na kuamua kuizalisha tena ili kukidhi mahitaji ya wateja wake na watanzania kwa ujumla.

“Leo ni siku ya furaha kubwa kwetu Serengeti breweries kuona umati mkumbwa wa watanzania mmehudhuria katika uzinduzi huu siku ya leo ambapo tuna irudisha tena sokoni bia yetu ya KIBO GOLD ikiwa na muonekano uleule, ladha ileile, na ubora uleule iyofanya bia hii kupata umaarufu mkubwa ilipokuwa sokoni miaka michache iliyopita” alisema Chonjo na kuongeza kuwa bia hiyo itauzwa kwa bei ya shs.1500 tu. Hali ambayo inaweza kuwa faida kwa watanzania wote wenye mapenzi mema na kampuni ya bia ya Serengeti.

Kwa upande mmoja wa wakongwe katika utumiaji wa bia ya kibo gold wakati inatengenezwa na na kampuni ya bia ya kibo breweries wakati ule kabla haijafa,bw Julius Nyaki ameishukuru na kukipongeza kampuni ya bia ya Serengeti kwa kurudisha bia hiyo sokoni ambapo sasa inarudi tena ikiwazalishwa na kampuni ya bia ya Serengeti kiwanda cha Moshi makoani Kilimanjaro na kuuzwa nchi nzima.

Sambamba na tukio hilo, kampuni ya bia ya Serengeti kupitia promotion inayoendelea maarufu kama VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO imekabidhi zawadi ya pikipiki mpya kwa mshindi wake bw. Vicent Lymo mkazi wa kibosh mkoani kilimanjaro aliyejishindia zawadi hiyo kupitia promotion hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...