Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 4, 2012

WASHINDI WENGINE WANNE WASHINDA ZAWADI ZA SBL,WAWILI WASHINDA GENERETA, MMOJA AJISHINDIA PIKIPIKI,HUKU MWINGINE AKIJINYAKULIA BAJAJ, ZAWADI ZOTE MPYA KABISA,



 Meneja wa bia ya Serengeti Lager Bw. Allan Chonjo wa pili kutoka kulia akiwasiliana na mshindi katika bahati nasibu ya Vumbua Dhahabu chini ya kizibo inayoendeshwa na kampuni ya bia ya Serengeti, Kulia ni Meneja mawasiliano wa SBL Imani Lwinga na kutoka kushoto ni Cheryl Vroom kutoka PWC, Tumainieli Malisa kutoka PWC na waliosimama nyuma kulia ni Joyce Mwijage Mratibu Rasilimali watu SBL na Abubakary Maggid kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha.
Ni katika promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO NA SBL.
Kampuni ya bia ya Serengeti leo imeendelea na droo ya tisa katika promosheni inayoendelea ya ‘VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO’ iliyochezeshwa katika ofisi za kampuni hiyo SBL zilizopo maeneo ya Oysterbay jijini na kuhudhuriwa na waandishi wa habari, wasimamizi kutoka Bodi ya Bahati Nasibu Tanzania, wadau kutoka ndani na nje ya kampuni hiyo, wakiwemo kampuni ya kuendesha Bahati Nasibu ya PUSH MOBILE, wahakiki na wakaguzi kutoka PWC-Price Water House Coopers.
Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia vinywaji vyake aina ya Serengeti premium Lager, Tusker Lager na Pilsner Lager inaendesha promosheni hiyo nchi nzima ambapo kwa mara nyingine washindi wane wameweza kuibuka na ushindi katika droo iliyochezeshwa leo asubuhi.
Akionge na wandishi wa habari wakati wa kuchezesha droo hiyo, meneja wa bia ya serengeti lager bw. Allan Chonjo amesema “ni wiki ya tisa sasa ambapo tunaendelea na promosheni yetu ambayo bila shaka watanzania wengi mmekuwa mkishuhudia watanzania wenzenu wakijishindia zawadi mbalimbali nakukabidhiwa pale walipojipatia zawadi hizo’ naendelewa kuwasisitiza wateja wetu na watatnzania wote kwa ujumla kuwa bado zawadi zipo nyingi na kwambakila mmoja wenu anaweza kushinda kama vile ambavyo wengine wanajishinadia
Washindi wetu katika droo hii ya tisa ni bwana Boaz Mtukula kutoka Mwanza ambaye ni mfanyakazi wa benki ya Twiga Bancorp mywaji wa bia ya Tusker Lager na bwana Richard Valerian kutoka Dar Es Salaam anayefanya kazi Bandarini mywaji wa Tusker pia ambao wote kwa pamoja wamejishindia jenereta mapya kabisa, na bibi Rahma Ally mkazi wa Temeke jijini Dar Es Salaam ambaye amejinyakulia pikipiki mpya mywaji wa bia ya Serengeti Premium Lager na Bwana Richard Mbizi mkazi wa Kimara jijini Dar Es Salaam amamejishindia bajaj mpya kabisa, zawadi zote kutoka SBL.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...