Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, June 18, 2013

'NYOTA NJEMA' YA SALMA SEGERE YAANZA KUTESA




Na Elizabeth John

MWANADADA anayetamba katika tasnia ya muziki wa Taarabu nchini, Salma Swed ‘Salma Segere’ ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Nyota Njema’ ambao umeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Mbali na kibao hicho mwanadada huyo alishawahi kutamba katika vibao vya Segere, Lindima, Alongore na vinginevyo ambavyo vimeimbwa na kundi la muziki huo la Wazazi Culture Troup ‘Segere Original’.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Salma Segere alisema anamshukuru mungu kazi hiyo inafanya vizuri katika tasnia ya muziki huo ikiwa ni pamoja na kupokelewa vizuri na mashabiki wa Taarabu nchini.

“Namshukuru mungu kazi hii imepokelewa vizuri na mashabiki wangu, kwani tasnia ya muziki sasa ina wasanii wengi sana hadi kazi yako ikikubalika ujue umefanya kazi nzuri na umeumiza sana kichwa,” alisema.

Alisema kwasasa yupo katika mchakato wa kuachia video ya kazi hiyo ambayo anaamini itafanya vizuri pia kutokana na mazingira ambayo ameyatumia kutengeneza kazi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...