Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, June 16, 2013

SHOO YA 'KIJANJA YA THE FINEST' MWANA FA YAWAPAGAWISHA MAKAMBA NA ZITTO UKUMBINI


Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Hamis Mwinjuma Mwana FA na Linah, wakiimba kwa pamoja jukwaani, wakati wa shoo yake ya 'The Finest' iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam jana usiku. Katika onyesho hilo lilihudhuliwa na baadhi ya Viongozi wa vyama vya Siasa pamoja na wasomi kibao kutoka Vyuo mbalimbali. Miongoni mwa wanasiasa walioonekana kwa haraka haraka ukumbini hapo ni pamoja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, aliyeketi na kuparty pamoja na Mbune wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
********************************
Halima Kambi, Dar
KATIKA Shoo hiyo ya 'Kijanja' pia ilihudhuliwa na wasomi kibao huku baadhi ya wabunge kama Zitto Kabwe na January Makamba wakiwa ni miongoni mwa mashabiki wajanja waliohudhuria katika shoo hiyo ya "kijanja" ya The Finest Kama Zamani iliyofanyika  katika Ukumbi Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam, jana usiku.

Mwana FA, pia alisindikizwa na na baadhi ya wasanii kama, Ben Paul, Linah, Maua, Dully Sykes na wengine kibao pamoja na bendi ya Njenje

Kiukweli show ilifana sana kutokana na utaratibu na mpangilio na maandalizi ya shoo yenyewe na MwanaFA aliweza kufanya yake jukwaani na kuwapagawisha mashabiki wake katika usiku ule.

Kutoka (kulia) ni Mbune wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akiwa na Mbunge wa Bumbuli (CCM) January Makamba, wakiwa ni miongoni mwa mashabiki wa Mwana FA, waliohudhulia shoo hiyo. Kushoto ni Mtangazaji wa Clouds FM, Gerald Hando.
 Mwana FA, akishambulia jukwaa kwa mistari ya kina.....
 Sehemu ya warembo mashabiki wa Mwana FA, wakijitahidi kunasa matukio kupitia simu zao za mkononi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...