Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, July 5, 2012

Mzee Ali Hassan Mwinyi atembelea maonyesho ya Sabasaba leo


Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Tanzania Ally Hassan Mwinyi(katikati) akiongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda kutembelea mabanda mbalimbali(leo) jijini Dar es salaam katika maonyesho ya 36 ya Kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Tanzania Ally Hassan Mwinyi(kulia) akiangalia mahindi yaliyopandwa kitaalamu  (leo) jijini Dar es salaam baada ya kiongozi huyo mstaafu kutembelea bustani ya mfano ya MAGEREZA  katika maonyesho ya 36 ya Kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Tanzania Ally Hassan Mwinyi akitopata maelezo juu ya miradi mbalimbali inayosimamiwa na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC)  jijini Dar es salaam baada ya kiongozi huyo mstaafu alipotembelea maonyesho ya 36 ya Kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Tanzania Ally Hassan Mwinyi akitoa maoni yake (leo) jijini Dar es salaam baada ya kiongozi huyo mstaafu kutembelea banda la MAGEREZA  kuona thamani za majumbani wakati alipotembelea maonyesho ya 36 ya Kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...