Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, July 19, 2012

NBC YAMKARIBISHA BOSI WA BARCLAYS AFRIKA NA KUFANYA MAZUNGUZO NA WATEJA WAO.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru
(kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza
wakishakana mikono wakati wa hafla iliyoandaliwa na NBC kwa wateja
wake wa makampuni jijini Dar es Salaam jana.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Afrika, Kennedy Bungani (kushoto)
akipiga picha na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula
Mfugale (katikati) na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Godfrey
Ndalahwa  baada ya kufanya mazungumzo na wafanyakazi wa benki hiyo na
baadhi ya wateja wa makampuni wa NBC jijini Dar es Salaam jana usiku.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru
(kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene
Meza (wa pili kushoto) katika  hafla iliyoandaliwa na NBC kwa wateja
wake wa makampuni jijini Dar es Salaam jana.  Wa pili kulia ni Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Barclays Afrika, Kennedy Bungani na Mkuu wa Kitengo
cha Wateja wa makampuni wa NBC, Minnie Adolf Kibuta. Bwana Bungani
awali alifanya mazungumzo na wafanyakazi wa NBC nchini ili kufahamiana
nao.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Afrika, Kennedy Bungani (kulia)
akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene
Meza katika  hafla iliyoandaliwa na NBC kwa wateja wake wa makampuni
jijini Dar es Salaam jana.  Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki
ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru. Bwana Bungani awali alifanya
mazungumzo na wafanyakazi wa NBC nchini ili kufahamiana nao.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Afrika, Kennedy Bungani (wa tatu
kushoto) akipiga picha na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NBC
Tanzania baada ya kufanya nao mazungumzo na baadhi ya wateja wa
makampuni wa NBC jijini Dar es Salaam jana usiku.
Mshauri wa Mahusiano wa NBC, Eddie Mhina (kulia), Meneja Chapa na
Matangazo, Aden Kitomari (kushoto), pamoja na mfanyakazi mwingine wa
benki hiyo wakiwa katika hafla waliyoandaa kwa wateja wao wa makampuni
jijini Dar es Salaam jana.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...