Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, August 16, 2012

NMB KARIBU YAKO WAKATI WA RAMADHAN


 Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NMB, Imani Kajula (kushoto), akimkaribisha Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Soraga katika futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki hiyo, Zanzibar. Anayeshuhudia ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Salie Mlay.
 Kamishina wa Polisi Zanzibar, Musa Ali Musa (wa pili kulia) akisalimiana na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NMB, Imani Kajula wakati wa futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wa NMB Zanzibar. Katikati ni Meneja wa NMB Zanzibar, Mluku Maggid.

Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Soraga (kulia) akipeana mkono na Ofisa wa Huduma kwa Wateja NMB Zanzibar, Haji Dau wakati wa futari ya wateja wa NMB wa Zanzibar. Katikati ni Meneja wa NMB Zanzibar, Mluku Maggid.
 Meneja wa NMB Zanzibar, Mluku Maggid akizungumza na wateja wa NMB waliofika katika futari iliyoandaliwa kwa ajili yao na benki hiyo.
Meneja wa NMB Zanzibar akizungumza na Meneja wa NMB Zanzibar, Mluku Maggid (kushoto). Katikati ni Meneja Masoko wa NMB, Shilla Senkoro.
Wateja wa NMB Zanzibar wakiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa wa NMB mara baada ya futari waliyoandaliwa na benki hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...