Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, August 11, 2012

Tigo kutanua wigo wa mtandao nchini koteTigo kutanua wigo wa mtandao nchini kote




9, Agosti 2012, Dar es Salaam. Kampuni ya simu za mikononi ya Tigo imeamua kujizatiti katika mpango wa upanuzi wa mtandao ili kuboresha huduma zake nchini.

Kama sehemu ya mikakati yake Tigo inapanga kuwekeza jumla ya dola za kimarekani shilingi milioni 100 mwaka huu ili kukarabati na kufungua vituo vipya nchini.Uwekezaji huu utaongeza ubora na kiwango ch

a upatikanaji wa mtandao wa Tigo. Upatikanaji wa matandao utakuwa mkubwa na rahisi nchi nzima, wateja wa Tigo watapata mtandao wenye kasi zaidi nchini kote.

Upanuzi huo unaotegemewa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu utasambaa kwenye mikoa yote 26 ikiwemo mikoa ya kanda ya ziwa, kusini na kaskazini, Mtwara, Iringa na Pwani na kuifanya Tigo kuwa mtandao ulionea zaidi nchini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...