Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, October 14, 2014

Dk Ndumbaro yamkuta, afungiwa miaka 7 katika soka


BAADA ya tetezi zilizokuwa zikizagaa kwamba huenda Mwanasheria wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Dk Damas Ndumbaro yupo kitanzini na huenda akaadhibiwa kwa kauli alizotoa hivi karibuni kuhusiana na makato ya 5% zilizotakiwa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, hatimaye imethibitika kuwa kweli.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia Dk Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha fedha.
Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam TV.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu, Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia,.
TFF imedai Ndumbaro amekanwa na klabu ingawa taarifa zinaeleza si kweli kwa kuwa viongozi wa klabu 12 walisaini kumpitisha kuwa wakili wao

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...